Watu wengi hudhani kuwa mwaka mpya wa kirumi husherehekewa na watu wote duniani. Wafuasi wa imani ya Bahá’í , kwa mfano, wanasherehekea mwaka mpya Machi 21 (siku hiyo huitwa NaW Ruz. Kalenda ya Ki-Bahá’í ina miezi 19 yenye siku 19. Imani ya Bahai ilianzishwa na Bahá’u'lláh. Wachina nao wana mwaka mpya wao. Sijui kama unajua kuwa miezi ya kichina ni majina ya wanyama. Kongoli hapa kwa undani zaidi. Nchini Thailand, mwaka mpya uitwao Songkran husherehekewa Aprili 13 hadi 15 kwa kurusha maji. Mwaka mpya wa Kikeltiki, Samhain, husherehekewa mwezi wa Novemba. Kalenda ya Kirumi ya zamani ilikuwa na miezi 10, na mwaka mpya ulianza Machi Kwanza.
Kalenda inayotumika katika nchi nyingi hivi sasa ni Kalenda ya Kiregori ambayo ilichukua nafasi ya Kalenda ya Juliani. Kanisa Katoliki lilipendelea kubadilisha kalenda ya Juliani kwasababu kadhaa, mojawapo ikiwa ni kufanya waumini wa kikristu washerehekee pasaka karika siku iliyokubaliwa na Baraza la Nikea. Huko Abisinia (Ethiopia) mwaka mpya (enkutatash) ulisherehekewa mwezi wa tisa tarehe 11. Kumbuka kuwa Abisinia iko nyuma miaka saba na miezi nane ya kalenda ya Kiregori (Giriligoloyo kwa wale waliosome Song of Ocol and Lawino) inayotumika katika nchi nyingi duniani hivi sasa. Kalenda ya Ethiopia ina miezi 13. Waislamu nao wana kalenda yao ambayo inafuata majira ya mwezi badala ya jua kama ilivyo kalenda ya kirumi. Kalenda hii ni pungufu kwa siku 11 tofauti na ile inayofuata majira ya jua. Mwaka mpya kwenye Uislamu huwa ni mwezi wa pili. Mwaka 2005 kwenye kalenda ya Kiislamu ni mwaka 1426. Mwaka wa Kiislamu unaanza toka pale mtume Muhammada na wafuasi wake walipokimbilia Medina toka Maka (mwaka 632 katika kalenda ya kirumi).
December 2004
Fri 31 Dec 2004
Fri 31 Dec 2004
Sherehe za mwaka “mpya” wa kirumi kule mtaani kwangu najua kama kawaida zilipamba moto kwa mayai viza na baruti. Sijui kama umewahi kupigwa na mayai viza. Mayai yaliyooza. Usiombe. Zaidi ya mayai viza, kuna wimbo maarufu (mchanganyiko wa kichagga na kiswahili) ambao nimekuwa nausikia kichwani kama vile niko nyumbani. Wimbo huu ni wa kuamsha wale waliolala wakati wa kupiga madebe na kurushiana mayai viza. Kaka yangu, Walter, kanikumbusha huu wimbo hivi majuzi:
Mwaka mpya Eeeeeee
Mwaka mpya kure ipfo mba (yaani: toka huko ndani)
Lekana na kitara kyo (yaani: achana na kitanda hicho)
Mwaka mpya Eeee
Nilitaka sana kupiga madebe ila nikawa na hofu ya kuitiwa askari na majirani! Unajua tena nchi za sheria kali.
Fri 31 Dec 2004
Kama hujawahi kumsikia huyu bwana, nenda hapa. Hata kama unamfahamu, nenda hapo kisha soma hotuba zake (hasa iitwayo African History: Lost, Stolen, or Strayed na pia The Mis-Education of the African). Kuna nyingine inaitwa How To Reverse the Brain Drain.
Fri 31 Dec 2004
Eti rais wa Tanzania 2005 atakuwa na nywele fupi wastani, pua yenye kuonekana, na upele! Sio utabiri wangu bali wa yule mtabiri maarufu Afrika Mashariki, Sheikh Yahya Hussein. Utabiri kamili huu hapa.
Wed 29 Dec 2004
Jarida la New African liliandaa orodha ya Waafrika 100 maarufu duniani katika toleo lake la Agosti/Septemba 2004. Tazama orodha yenyewe kwa kwenda hapa, hapa, hapa, na hapa.
Wed 29 Dec 2004
Niliwahi kukutaka utege sikio kusikiliza kipindi cha AFROWORLD kinachoendeshwa na Mtanzania Nambiza Joe Tungaraza (DJ Joe) toka Australia kupitia Radio Adelaide 101.5 kila jumamosi. Masaa niliyoweka wakati ule ni ya Australia, ambapo ni saa 10:30 usiku hadi saa sita usiku. Leo naweka masaa ya sehemu nyingine ili muweze kukifuatilia. Hiki ni kipindi cha matukio na muziki kuhusu Waafrika (Afrika na Ughaibuni). Muziki aina mbalimbali kama Makossa, Zouglou, Rhumba, Kwaito, Rai, Highlife, Reggae, African hiphop unatumbuizwa. Na pia mjadala wa matukio ya kisiasa, kijamii, kitamaduni, na kiuchumi yanayohusu Waafrika.
Unachotakiwa kufanya ni kwenda kwenye tovuti ya Radio Adelaide kila jumamosi: www.radio.adelaide.edu.au na ukishafika hapo kongoli palipoandikwa “Listen Online.”
Masaa ndio haya (shukran Tunga):
Walioko Marikani: Midwest/East Coast: Saa 1 asubuhi.
West Coast: Saa 10 alfajiri.
Johannesburg: Saa 8 mchana.
DarEsSalaam: Saa 9 Alasiri.
London: Saa 6 mchana.
Amsterdam: Saa 7 mchana.
Oslo, Stokholm, Copenhagen : Saa 7 mchana.
Helsinki: Saa 8 mchana.
Wed 29 Dec 2004
Kuna rafiki yangu anapenda sana masuala ya afya na uhai. Kanikumbusha kuwa ni vyema nikawa pia najadili mambo hayo hapa bloguni. Hatuwezi kuwa kwenye mapambano dhidi ya utumwa wa fikra, udhalimu, na ufisadi wa watawala wetu bila kuwa watu wenye afya. Leo nitazungumzia maji.
Ninafahamu watu wengi sana ambao hawana tabia ya kunywa maji hadi wasikie kiu. Au wakiwa na kiu watakunywa sumu kali iitwayo soda. Au watakwenda baa kupata “udirinki.” Maji ni muhimu sana kwa afya yako. Kwanza kabisa usifikiri kuwa kazi ya maji ni kukata kiu. Ukisikia kiu ujue kuwa mwili wako umeishiwa maji kiasi ambacho umeamua wenyewe kukushtua. Kiu ni njia ya mwili kukwambia, “Rafiki, mbona umenisahau?” Kwa maneno mengine, hutakiwi uwe na kiu hata siku moja. Kunywa maji hata kama huna kiu ili usipate kiu hata siku moja. Kwa siku usikose si chini ya bilauri nane. Ukitaka kujua maji yalivyo muhimu mwilini, fahamu mambo haya:
Asilimia 70 ya mwili ni maji, asilimia 70 ya ubongo ni maji, asilimia 80 ya damu ni maji.
Wed 29 Dec 2004
Umuhimu wa blogu unajionyesha hivi sasa kutokana na maafa yaliyotokana na tetemeko la baharini (tsunami) huko Asia. Wana blogu hawako nyuma. Soma habari hii. Mwanablogu huyu kaweka na picha za video. Ukienda hapa utaona pia picha na video za maafa haya.
Tue 28 Dec 2004
Kuna tovuti hii nzuri mno ya chuo kikuu cha Stanford kwa wale wanaofuatilia masuala ya utumwa, biashara ya utumwa, na malipo kutokana na madhara ya biashara hiyo (reparations). Kongoli hapa
Tue 28 Dec 2004
Ninajiuliza maswali haya kila mara: Ni lini Tanzania itaachwa kuitwa nchi masikini? Ni lini Tanzania itaacha kuwa nchi
inayoendelea na kuwa nchi iliyoendelea? Hivi hiyo siku itakaa ije?Kuna wakati huwa ninasita kusema kuwa Tanzania ni nchi inayoendelea. Kuendelea sio neno tu. Kuendelea ni hali ambayo unaweza kuipima. Karibu kila kipimo cha maendeleo ukikitumia, unaona kuwa Tanzania inarudi nyuma badala ya kwenda mbele. Kwa mfano siku zinavyokwenda wastani wa umri wa Mtanzania kuishi hapa duniani unapungua. Yaani kama wewe ni mtanzania unayeishi Tanzania, mauti utaikaribia kwa haraka sana! Najua inatisha, nisiseme?
Kwahiyo utaona ingawa inachukuliwa kuwa mataifa hapa duniani yamegawanyika kati ya yale
yanayoendelea na yaliyoendelea, ukweli ni kuwa kuna mataifa mengine yasiyoendelea, yaliyosimama na yanayorudi nyuma!Haya, turudi kwenye swali la msingi. Kwanini ajira ni vigumu kupatikana Bongoland? Isome barua pepe ninayoizungumzia upate jibu la kwanini hakuna ajira Tanzania:
Anapomaliza kuoga kwa sabuni iliyotengenezwa Kenya, anavaa shati lililotengenezwa Uingereza na suruali ya dengirizi iliyotengenezwa Marekani na viatu vya Kimarekani vilivyotengenezwa na wafanyakazi wa ujira mdogo huko Vietnam. Anakunywa chai kwenye meza iliyoagizwa toka Dubai na kula mayai yaliyokaangwa katika kikaangio kilichotengenezwa India. Sahani, kijiko na kikombe anavyotumia vimetoka China.
Anafungua redio yake kisasa iliyotengenezwa Taiwan huku akifungua kitabu chake cha kumbukumbu kilichotengenezwa Italia ili aweze kupanga ratiba yake ya siku kwa kalamu toka Uingereza.
Anapomaliza kupanga ratiba yake ananyanyua simu yake ya mkononi toka Japan na kuondoka kuelekea kwenye kituo cha basi ambako anapakia basi lililotengenezwa Japan na kununuliwa Dubai.
Jioni inapowadia anarudi nyumbani akiwa mchovu kabisa. Anaketi kwenye viti vilivyotengenezwa Singapore na kuanza kutazama kipindi cha luninga kilichotayarishwa Marekani kwenye luninga iliyotengenezwa Taiwan. Wakati akitazama luninga anajiuliza sababu inayofanya iwe vigumu kwake kupata kazi. Haelewi.
Tue 28 Dec 2004
Wazalendo wote, wana wa nchi, wazawa, wana mapinduzi, wakereketwa, wafurukutwa, wana ngangari, wana ngunguri, wana apollo (kule Mererani), vijana wa kule kwa mzee Jomo na “baba” Moi (sasa?), marastafari, vizabizabina, bila kumsahau mshikaji Joji Dabliyuu Kichaka, Wana mageuzi na mageuzo, wapiga debe, majangili yanayovaa kofia ya “uongozi,” makaburu wanaoitwa “wawekezaji,” polisi wanaokamata wahalifu huku nao ni wahalifu, wahubiri wanaotangaza wokovu wakati tunahitaji mapinduzi, mahakimu wanaohukumu wala rushwa huku nao wanakula rushwa (mbele, nyuma, kushoto, na kulia)…bila kuwasahau wana mapanga sha sha sha…! NIMERUDI. Samahanini kwa ukimya.
Bado siamini kuwa wale jamaa wenye ngozi isiyo na kemikali za melanin (Wayoruba wa Nigeria huwaita, “watu waliochubuka”) waliomuua dada yetu wameachiwa!
Hiyo baadaye. Ngoja nitafute kitu cha kwanza cha kukupa. Nina mambo yamejaa vyungu kumi na mbili. Nitaanza kupakua chungu namba saba.
Fri 24 Dec 2004
Fri 24 Dec 2004
Umeisikia Skype? Simu ya bure ya Intaneti. Piga kokote duniani. Usitoe hata “sumni.” Jaribu ujionee mwenyewe. Bofya hapa.
Fri 24 Dec 2004
Wale wazee wa mahisia. Wale wazee wa marege nendeni hapa. Kula muziki tani yako. Jaribu kusikiliza rege “roots” nzito hasa za Steel Pulse na Groundation.
Fri 24 Dec 2004
Kuna siku nilisema kuwa ningekuwa na uwezo ningefanya binadamu waweze kuendesha magari wakiwa wamelala! Hii ingenisaidia usiku wa leo wakati nikielekea Vermont, mwendo wa masaa kumi na kitu…kama hakutakuwa na theluji. Kumbe kwa uwezo wa teknolojia huenda ikawezekana siku moja. Tazama hapa.
Kingine nilichosema ni kuwa ningekuwa na uwezo ningefanya binadamu tuweze kusoma tukiwa usingizini! Na pia ningeongeza masaa ya siku, yaani siku iwe na masaa zaidi ya 24.
Usishangae mbona mawazo ya ajabu ajabu namna hii, ukiwa ughaibuni lazima mawazo kama haya yakujie!
Fri 24 Dec 2004
Kawaida sina tabia ya kuapa. Lakini leo naapa. “Hakya” nani vile…nikatike kichwa (Nalamba udongo na kulamba kidole kisha kukielekeza mawinguni tunakoamini ndio aishipo muumba). Angekuwa ni kabwela, mlalanjaa, ngozi nyeusi, mzawa, mzalendo kama wewe na mimi ametuhumiwa kuua angeonja joto ya jiwe lupango hadi amani ipatikane Mashariki ya Kati.
Faili lingepotea.
Tungeambiwa, “ushahidi unaendelea” kwa miaka mitano hata kumi.
“Vizibiti” vingepotea.
Baadhi ya mashahidi wangetoweka.
Wengine wangekufa.
Mara hakimu angefiwa.
Mara angepata dharura.
Mwendesha mashtaka angeumwa. Angepona. Angeumwa. Angepona.
Mwendesha upelelezi angehamishwa kituo.
Mwendesha upelelezi mpya angehitaji nusu mwaka au mwaka mzima kupitia kesi….
Ingekuwa balaa, nuksi, mkosi, bahati mbaya, uzembe, utumbo, ubadhirifu, rushwa, ufisadi …taja mengine.
Huyo ni mwenzetu.
Lakini wanapokuwa ni wale jamaa tunaowaabudu ambao mungu, yesu, na malaika wanafanana nao, na hata miti ya krisimasi tunaiwekea pamba ili iwe kama hali yao ya hewa ilivyo (hali yao ya hewa ina uungu fulani…!).
Akiwa ni jamaa mwenye damu ya jamaa waliomhadaa Mangungo wa Msovero…
unajua kitakachotokea.
Kama hujui…Hebu tazama.
Thu 23 Dec 2004
Wale wazee wa hisia wanaopenda kula marege (hasa wachagga na vishuu wote wa Arusa) waende hapa watasikiliza miziki hadi watakoma
Thu 23 Dec 2004
Nakumbuka ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya tisini nilipomuona babu Burning Spear kwenye video kwa mara ya kwanza. Sitasahau. Wimbo ulioningia ambao alikuwa akiuimba kwa hisia huku akizunguka huku na kule jukwaani ni ule anaouliza, “Unakumbuka enzi za utumwa?” Nami nakwambia kama hukumbuki, unapaswa kukongoli hapa.
Thu 23 Dec 2004
Je unafahamu kuwa krisimasi nchini Abisinia (Ethiopia) husherehekewa tarehe 7 Januari? Krisimasi nchini humo huitwa Ganna.
Labda ulikuwa pia hufahamu kuwa mwaka mpya nchini humo ambao huitwa Enkutatash, husherehekewa tarehe 11 Septemba. Absisinia hufuata kalenda ya Juliani ambayo ina miezi kumi na mbili ya siku 30 na mwezi mmoja (wa kumi na tatu) wenye siku tano! Kalenda hii, Juliani, iko nyuma kwa miaka saba na miezi nane ya kalenda ya Kiregori ambayo hutumiwa na mataifa mengi duniani.
Thu 23 Dec 2004



