NEWS: Discount viagra europe Discount phentermine prescription Discount viagra perscription drug Order phentermine on line? 92 accepted cod phentermine Compare viagra prices, Pharmacy online phentermine Purchase tramadol online. Phentermine sites that ship cash on delivery Viagra retail discount Home made viagra Valium vs xanax Xanax no prescription Viagra sales online Erection viagra Free viagra without prescription Phentermine fda Xanax withdrawl Effects phentermine side strong Information viagra woman What does phentermine do to your heart Long term phentermine use Viagra testimony Phentermine very cheap Buying phentermine Cialis pill? Discount online phentermine Buy cheap phentermine yellow Tramadol hcl tab Phentermine hydrochloride ship to missouri: Buy viagra prescription online Compare phentermine prices Cialis compare levitra viagra Picture of generic xanax Tramadol uses Recreational viagra use Generic india viagra Cheap viagra generic Cialis drug Natural phentermine Phentermine cheapest price 5 no perscription! Cialis and pomegranate interaction Viagra for woman? Ionamin phentermine Cheapest xanax online! Xanax drug interactions Buy cod phentermine Phentermine online Methadone and xanax Recreational viagra Viagra online sales Mexican phentermine Cod tramadol! Phentermine mexican pharmacies online Phentermine pictures Cheap phentermine without a prescription Compare viagra cialis levitra. Xanax master card Long term effects of xanax, Viagra cialis levitra comparison dosages Does viagra woman work 5 in round white tablets no imprint code 50 mg viagra Phentermine shipped cod Phentermine for less Viagra information Phentermine free consultation? Viagra kaufen Is tramadol a narcotic Cheap quality viagra Phentermine and topiramate for weightloss Diet loss phentermine pill weight Diet phentermine pill sale Kevin harvick viagra Xanax withdrawls Purchase viagra online Cialis new viagra. Viagra for woman information Online ordering viagra Viagra prescription uk Buying phentermine: Can i take xanax with zocor and procardia Phentermine overnight Does viagra work Low natural resources for the drug phentermine Viagra treatment migraine headache Buy in online uk viagra, Apcalis cialis 180 phentermine Black market costa rica pharmacy phentermine no imprint code Buying tramadol online Loss phentermine story success weight How much weight will you lose on phentermine Online xanax prescription Cialis compared to viagra Paxil with phentermine interactions Xanax addiction treatment. 0 buy by popl powered viagra wordpress Cheap tramadol 180 Viagra in woman Lethal doses of klonopin and xanax Stopping xanax Cialis overnight! Phentermine and urine drug screen Smoking xanax: Ingredient phentermine Saturday delivery phentermine Viagra prescription medication Free cialis 25 mg Viagra uses Xanax detoxification Viagra pictures Pfizer viagra online Online adipex phentermine prescriptions. Side effects of tramadol hydrochloride On line prescription viagra 100 phentermine Female spray viagra Tramadol hc Free viagra sample I need to find cheap phentermine delivered to fl Online pharmacy phentermine xenical meridia Compare phentermine prices Canada cialis generic? Xanax shipped cod No perscription xanax cheap Acquisto cialis Generic india viagra Buy cheap purchase uk viagra Viagra price Online phentermine pharmacy best cheapest Tramadol 50mg. Buy viagra online get prescription Addiction recovery xanax, Price for generic viagra Diet inexpensive phentermine pill Generic viagra canada No prescription phentermine Phentermine withdrawal symptoms Cheap viagra order online Cheapest viagra price Phentermine online doctor prescribed? Buy cialis uk Fast delivery phentermine, Keyword prescription qoclick tramadol without Tramadol dog Phentermine wholesale Snorting phentermine Discount phentermine online Tramadol online Cheap tramadol no prescription Cialis comparison levivia viagra Cheapest viagra online 92 accepted cod phentermine Cheap phentermine with online consultation Viagra alternatives uk Buy prescription tramadol without Buying viagra in the uk Xanax description Oxycontin xanax bars perclesept and lortab wha Generic viagra cialis Generic lowest price viagra Phentermine at cost with no prescription Picture of xanax pill Phentermine shortage Phentermine cheap free shipping Phentermine yellow 30 mg Addiction tramadol Tramadol hydrochloride tablet Phentermine cod delivery Online phentermine order Cyber pharmacy viagra Dangers of phentermine heart Buy cheap tramadol Xanax alcohol Cialis generic Tramadol prescription Free phentermine prescriptions 50 mg viagra Phentermine studies Viagra and levivia Phentermine feedback How long between phentermine and meridia Low cost phentermine Phentermine and topiramate for weightloss Tramadol hc Viagra overnight delivery Phentermine success stories Viagra cheap prescription Tramadol hydrochloride capsules Free shipping phentermine Diet pill addiction phentermine? Generic cialis soft tabs Side effects of xanax xr: Phentermine quick Buy xanax on line How long does xanax stay in the system Importing cialis from canada to us Buy cheap domain onlineatspacecom xanax Phentermine and diet pill

January 2005


JIBINI = CHEESE

Binadamu tuna tabia za aina mbalimbali kuhusiana na vyakula. Kuna watu wasiokula nyama kutokana na sababu mbalimbali kama za dini au afya. Hawali chochote kinachotembea ardhini, ruka juu ya nchi, kuogelea baharini (samaki). Hawa wanaitwa ni wala majani, mbegu, na matunda, kwa kiingereza “vegetarians.” Kuna wengine wasiokula sio tu nyama bali chochote kile kinachotokana na wanyama. Hawa kwa kiingereza (bado natafuta jina la kiswahili) wanaitwa vegans. Tofauti ya “vegetarians” na “vegans” ni kuwa “vegetarians” huwa wanakula mayai, jibini, kunywa maziwa, n.k. Wakati “vegans” hawagusi hivyo vitu na wengine wala hawavai nguo, mikanda, viatu, au kubeba mikoba iliyotengenezwa kutokana na ngozi za wanyama. Nenda hapa na hapa kupata undani wa “veganism.”

Halafu kuna wengine ambao ndio funga kazi. Hawa ni wala vyakula vibichi. Kwa kimombo wanaitwa “raw foodist.” Hawa hawapiki chakula hata siku moja. Kwa maana hiyo hawahitaji kuwa na jiko majumbani mwao! Inaaminika kuwa hakuna njia inayoharibu virutubisho vilivyomo ndani ya chakula kama kupika. Watu wengi hawafahamu kuwa binadamu walitembea juu ya dunia hii kwa miaka mingi sana kabla moto haujagunduliwa. Kwahiyo wanachofanya ma-raw foodist sio jambo geni. Wanadamu walikuwa wakila vyakula vibichi kwa miaka mingi sana. Na wako wanaoendelea hadi leo. Wasome hapa.

Kuna kundi pia la wanaoishi kwa kula matunda tu. Wala matunda wanaitwa “fructarians.” Wasome hapa.

Kuna watu wengine wanaitwa “freegans” ambao wao chakula wanachokula ni kile ambacho kimeachwa, kusazwa, au kutupwa na watu wengine. Wasome hapa.

Kuna watu wengine ambao wanachukulia vegans na makundi mengine kuwa kama makundi madogo ndani ya mfumo mzima wa vegetarianism (ulaji wa mboga, mbegu, na matunda). Uchambuzi wangu wa makundi haya naweza kusema kuwa ni wa rahisi na juujuu kuliko ilivyo hasa. Tembelea hapa usome zaidi juu ya “vegetarianism” na mahusiano ya mfumo huu wa maisha na dini mbalimbali.


Kuanzia sasa nitakuwa ninatumia teknolojia ya blogu ya sauti (audioblog) pamoja na hii ya maandishi. Kwahiyo hata nikiwa safarini, porini, milimani, vijijini, chooni, n.k. naweza kutumia simu ya mkono kuwasiliana nanyi ndugu zangu.

this is an audio post - click to play

Tafadhali kama kuna mtu mwenye limao au ndimu anipatie ili niwe nakula kabla sijatembelea tovuti ya bunge la Tanzania na ile ya ikulu. Kila ninapotembelea tovuti hizi mbili za nchi inayojulikana kwa lugha ya Kiswahili, lugha ambayo ndio inajulikana na kutumiwa na wakesha hoi masaa 24, ninakaribia kutapika kama mtu aliyemeza konokono kwa bahati mbaya. Sijui kama ni mimi peke yangu ninayehoji sababu ya tovuti hizi kuwa katika lugha ya akina Tony Blair na Malkia Lizabeti na sio lugha inayotumiwa na akina Rafaeli (ndio, yule Rafaeli wa kwenye wimbo wa Saganda!), Kalubandike, Mama Giresi, Masanja, Zabuloni, n.k.
Ukitembelea tovuti ya ile ikulu iliyojengewa kuta kama ule wimbo wa Paul Ndunguru usemavyo, “Wanajenga kuta kuzuia wezi wenzao…,” unakuta kuna salamu za mwaka mpya wa kirumi wa 2005 ambazo zimetolewa na Rais wa Tanzania kwa wananchi wa Uingereza!
“Inakuwaje rais wa Tanzania atoe salamu kwa wapiga kura wa nchi nyingine na sio wananchi wake?”
Usiniulize. Sina jibu.
Na kama huniamini nenda hapa ujionee mwenyewe. Ukiwa umefumbua macho utaelewa kwanini nimesema kuwa salamu ya Rais ni kwa ajili ya wananchi wa Uingereza.
Leo sio mara yangu ya kwanza kulalamika juu ya hili. Na sio ya mwisho. Lazima tukomeshe huu mchezo unaochezwa na waliozama katika bahari ya utumwa wa fikra.
Rafiki yangu mmoja anayesoma Afrika Kusini kaniambia kuwa tovuti hizi zimegharamiwa na shirika la maendeleo la “umoja” wa mataifa (UNDP). Kuna uwezekano kuwa tovuti hizi zinatumia lugha yao kwakuwa “msaada” umetoka kwao. Hili neno “msaada” karibu nitalifuta kabisa kwenye misamiati yangu. Naona limepoteza maana yake siku nyingi.

Hatimaye yule mwandishi wa BBC, Ivan Noble, ameweka nukta ya mwisho katika kitabu chake cha kumbukumbu kilichokuwa mtandaoni kikionyesha maisha yake baada ya kupatikana na kansa ya ubongo. Ameweka nukta ya mwisho baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya. Msome.
Kitabu chake cha kumbukumbu kilikuwa kikisomwa na watu 100,000 kwa siku.

Jana nilipandisha makala moja mpya: Elimu ni Utumwa? Leo nimeweka nyingine tatu ambazo niliziandika nyuma kidogo. Zote hizi tatu zilitoka kwenye safu yangu ya Gumzo la Wiki. Makala ya wiki hii nitaiweka baada ya kutolewa gazetini. Makala za leo ni: 1. WEWE MWENYE RASTA NJOO! 2. NANI ATAWAKAMATA POLISI? 3. YESU/ISA NA WATANZANIA

Sankofa, habari za masiku? Nitajibu waraka wako ambao umeniandikia muda kidogo. Nimesoma habari ya DJ Spooky nikakukumbuka. DJ Spooky (Paul Miller): anafanya jambo ambalo limenipendeza sana. Ameuganisha u-DJ na utengeneza filamu. Kama jinsi ma-DJ wanavyochanganya muziki (nyimbo, vyombo, vibwagizo, n.k.) ndivyo DJ Spooky anafanya. Ameitengeneza upya ile sinema ya Birth of a Nation, matokeo yake imepatikana filamu ya Rebirth of a Nation.
Pia utaona kazi kwenye tovuti yake mradi wa A Different Utopia ambao ni mchanganyiko wa muziki, insha, teknolojia ya flash katika kuelezea falsafa ya Fela Kuti kupitia makazi yake ambayo aliyaita Jamhuri ya Kalakuta.

Ninatamani mambo mengi. Mojawapo ni hili: Ninatamani sana siku moja nikutane ana kwa ana na wananchi wanaoitwa, “wananchi wenye hasira kali.” Hawa ni wale ambao wakisikia, “mwizi!” damu inawachemka, wanatafuta mawe, mitaimbo, nyundo, matairi, bisibisi, patasi, petroli, na viberiti ili wamuue mtu ANAYEDAIWA kuwa mwizi.

Ukikuta hawa wananchi wenye hasira kali wanaua binadamu mwenzao, mtafute aliyewasha kiberiti, kisha muulize, “Hivi jamaa kaiba nini?” au, “Kamwibia nani?” Utasikia majibu ya ajabu kweli.
“Ah, jamaa wanasema kaiba mtaa wa pili.” Atakujibu. Anayekujibu hivyo ndiye aliyewasha moto uliomteketeza marehemu. Ukimuuliza akutajie majina ya hao ” jamaa wanaosema” kuwa kaiba mtaa wa pili, atakachoweza ni kuwataja kwa jina la “jamaa.” Atasema, “Jamaa waliomkamata ndio walimuona.”
Jamaa ndio akina nani hao?
Hajui.

Msimamishe yule aliyemwangushia tofali kichwani lililomfanya marehemu atoe damu puani na machoni. Muulize swali, “Kafanya nini marehemu?”
Atakujibu, “Wamezidi hawa!”

Nimesema kuwa ninatamani sana kukutana na “wananchi wenye hasira kali.” Nataka kuwauliza swali hili: Wezi wa kuku mnawapeleka jela. Wezi wa shilingi 1,000 mnawapiga mawe na kuwachoma moto hadi kufa, JE WEZI WA MAMILIONI YA UMMA MNAWAFANYA NINI?
Hizo “hasira kali” zinakuwa wapi wakati nchi ikipigwa mnada??

Natamani sana sana kukutana nao. Ukikutana nao naomba nisaidie kuwauliza swali hilo kisha nitumie majibu.Yesu akauambia umati, “Asiye na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe.” Mara wakaondoka mmoja mmoja na kumwacha na yule mwanamke aliyeshatakiwa kwa uzinzi.

Nimeweka makala mpya toka kwenye safu yangu ya Gumzo la Wiki katika gazeti la Mwananchi. Makala inaitwa Elimu ni Utumwa? Kama kawaida iko kwenye kona ya makala zangu, upande wa kuume, chini ya picha yangu. Kichwa cha makala hii kilikuwa ni hiki: Elimu ni Ufunguo wa Utegemezi. Nimekibadili kuwa swali: Elimu ni Utumwa? Makala hii ilipaswa kusomwa kama sehemu ya pili ya makala nyingine kuhusu usomi na wasomi. Nimeamua kupeleka mambo kinyume. Nimeanza kukupeni sehemu ya pili kisha niwapeni sehemu ya kwanza!

Kuna mafunzo ya aina mbalimbali kwa njia ya video kwa wale wanaopenda masuala ya teknolojia. Kongoli hapa.

Terms of reference = Hadidu za rejea
Vinegar = Siki
Furniture = Samani

Kumbuka kuwa Ice ni barafu na snow ni theluji.

Kumbe hivi karibuni Watanzania tulioko ughaibuni tutaweza kwenda Kigoma na kurudi ughaibuni siku hiyo hiyo. Itakuwa hivyo kama yaliyosemwa kwenye habari hii sio si-hasa bali ukweli.

Kuta zile zinazojengwa na wa-twawala (yaani watawala au “viongozi”) kuzuia uhuru wa fikra na maoni zinapoanguka lazima tushangilie. Kama ilivyotokea hapa.

Ndio kunakucha katika ulimwengu wa blogu za Kiswahili. Kuna mwanablogu mpya wa Kiswahili. Huyu ni Innocent Kessy, Mtanzania aliyeko masomoni nchini Uganda. Mtembelee katika blogu yake ya Dira Yangu hapa.

Kuna mwandishi mmoja wa gazeti la The Christian Science Monitor ambaye ana bloguluninga. Yuko Afrika. Sijaitazama vizuri. Itembelee. Bloguluninga inakuja juu sana hivi sasa. Nimepata habazi zake toka kwa Ethan.

Kutokana na maombi ya wengi kuhusu makala za uchambuzi na falsafa za Padri Karugendo, ambazo hutoka kila alhamisi katika gazeti la RAI (nguvu ya hoja) nchini Tanzania, ninaweka kona maalum kwa ajili ya makala zake. Hivyo mtaanza kumsoma hivi karibuni.

Ninapenda kutangaza kuwa mwezi ujao, ambao ni mwezi wa historia ya watu weusi hapa Marekani, kutakuwa na mfululizo wa mambo mbalimbali ya kukomboa fikra zetu katika kuenzi historia yetu. Afadhali ukose kuja hapa mwaka mzima ila sio mwezi wa pili!


Kuna mshairi mwingine ambaye staili yake ninaipenda sana. Napenda wasiomfahamu, wamfahamu. Huyu ni Saul Williams. Ukifika kwenye tovuti yake unaweza kusikiliza baadhi ya mashairi yake. Unaweza pia kusikiliza na hata kuchota CD yake ya hivi karibuni. Pia unaweza kutazama baadhi ya video zake. Nenda hadi mwisho wa ukurasa wa kwanza na ubonyeze panaposema: The Work. Unaweza ukawa umetazama filamu ya Slam ambayo aliicheza.

Nenda kwenye blogu ya Furahia Maisha Yako. Kuna habari ya Sumaye kushangaa mijinaume inayopenda ngono kiasi ambacho inatoa machozi kabisa, na hata kutumia maelfu kwa ajili ya vitanda katika hoteli za kifahari lakini shilingi 100 ya kondomu hawatoi!
Ukifika hapo usiache kusoma sheria za kuvaa suti. Nimecheka kwa sauti, nadhani majirani wamepata mshtuko. Mwanablogu huyu alinichekesha wakati ule alipoandika sifa za uswahili.

Sikuwa najua kuwa kuna watu wamekuwa wanablogu safari yao ya kupanda mlima ambao hauko mbali na nilipozaliwa. Blogu ya hao mabwana ni hii na habari yenyewe nimeikuta sebuleni kwa Mawazo na Mawaidha.

Next Page »