April 2005
Thu 28 Apr 2005
Thu 28 Apr 2005
Kwa wale wanaomjua mungu kwa jina lake ni Allah au Yehova tu, nenda hapa.
Thu 28 Apr 2005
Thu 28 Apr 2005
Fuata kiungo hiki hapa usome habari mbalimbali kwa kiingereza kuhusu teknolojia ya blogu.
Tue 26 Apr 2005
Kama wewe ni mtunzi wa vitabu na hutaki kupigapiga hodi kwa wachapaji au huna fedha za kuchapa kitabu chako mwenyewe, teknolojia ya uchapaji mtandaoni inakuwezesha kuchapa kitabu chako bure. Unabisha? Nenda hapa.
Tue 26 Apr 2005
Mtoto wa aliyekuwa mwizi mkuu wa nchi ya Togo kwa karibu miaka 40, Faure Gnassingbe, amehalalishwa kuendelea kazi ya wizi aliyoianza baba yake miongo mingi iliyopita. Soma hapa.
Tue 26 Apr 2005
Hii hapa ni blogu ya aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Uswidi.
Mon 25 Apr 2005
Sun 24 Apr 2005
Tazama filamu ya jamaa wa Creative Commons (Afrika Kusini) inayohusu mzunguko wa maarifa. Iko Hapa.
Sun 24 Apr 2005
Kule Kenya wenye simu za mkono wanaweza kutafuta kazi kwa kutumia huduma ya ujumbe wa maandishi. Bonyeza hapa.
Sun 24 Apr 2005
Sun 24 Apr 2005
Mapinduzi ya kila aina yanatokea kila upande. Wananchi walichachamaa na kuandamana (kule Jojia, Ukraine, Lebanoni serikali zikaanguka. Sasa huko Ecuador nako maandamano ya umma yameangusha serikali. Soma hapa, hapa , hapa na hapa. Wapi kunafuatia? Zimbabwe? Kenya? Tanzania? Marekani?
Sun 24 Apr 2005
Polepole ndio mwendo, walituambia wahenga. Blogu za lugha za Kiafrika zinaongezeka kadri siku zinavyokwenda. Ukiacha blogu za Kiswahili, kuna blogu moja ya Ki-Bambara (Mali) ambayo bado ninatafuta anuani yake. Halafu kuna blogu nyingine ya rafiki yangu, Mokhtar, inakuja kwa lugha ya Ki-Berber. Kuna blogu ya Ki-Shona. Bonyeza hapa.
Sun 24 Apr 2005
Dalili za kuwa dunia imeingia kwenye mapinduzi ya zana mpya za mawasiliano ni nyingi. Ila mojawapo ni hii: papa mpya wa dini ya kikatoliki ya Roma ana anuani ya barua pepe. Kama unataka kuandikiana naye, mwandikie kwa anuani hii: benedettoxvi@vatican.va
Sun 24 Apr 2005
Msomaji wangu wa siku nyingi, Patrick Mwasomola, kaandika dakika chache zilizopita kwenye kitabu cha wageni. Anatukumbusha maneno ya unabii ya Bob Marley katika wimbo wake wa Uvamizi wa Usiku (Ambush In the Night). Hivi ndivyo alivyoandika:
Nimemkumbuka Bob Marley leo anatukumbusha kuwa:
WAMEKUWA WAKITULAGHAI
KWA SPEA PATI, PESA, NA BUNDUKI ZAO…
*****************************************
Katika wimbo huo Bob alikuwa akizungumzia mabepari ambao leo hii tunawaita wawekezaji na wahisani. Kama una rekodi ya Bob kasikilize wimbo huo vizuri.
** Neno jingine la kiswahili la Spea Pati ni Vipuli.
Wed 20 Apr 2005
Nilipanga kublogu habari hii leo asubuhi lakini kwa kuwa asubuhi la leo lakini kutokana na sababu za kiufundi nilishindwa. Ninadiriki kusema kuwa katika ulimwengu wa blogu za Kiswahili ndio kumekucha sasa. Blogu niliyokuwa niliyokuwa nikiisubiri kwa muda mrefu sana imejitokeza toka matawi ya chini huko Australia. Hii ni blogu iitwayo Mwandani ya Joseph Nambiza Tungaraza, Mtanzania anayeishi nchini Australia. Hivi ndivyo anavyosema mwenyewe juu ya blogu hiyo: Mwandani keshaingia ulimwengu wa blogu.Humu ndani ya blogu hii nitapeperusha mawazo kadiri yanavyovinjari kichwani – siasa, utamaduni, sanaa, mapenzi, ubinadamu, mahusiano ya watu wa rangi tofauti, matabaka tofauti, mataifa tofauti - kadhalika maswala ya haki na demokrasia yetu Waafrika.
Ukienda katika blogu hiyo utakutana na mjadala mfupi kuhusu kifo cha Papa Yohane Paulo. Nimependa sana hoja anazojadili. Nimependa kwa mfano pale anaposema kuwa kama uchaguzi wa Papa ni uchaguzi wa mwakilishi wa Mungu duniani, hakuna haja ya watu kutaka eti Papa atoke sijui Afrika au Marekani ya Kusini. Ninakubaliana naye kabisa maana kwa mungu sisi wote ni familia moja. Hakuna masuala ya rangi au jiografia. Haya, tembelea blogu ya Mwandani (au tuseme mtembelee Tungaraza) hapa.
Wed 20 Apr 2005
Nitaongelea kwa undani mazungumzo yetu baadaye. Kwa sasa ningependa umfahamu Zuckerman. Ethan Zuckerman ni mtafiti katika chuo kikuu cha Harvard. Habari zaidi juu yake hapo Harvard na mengine ambayo amewahi kufanya hapa. Soma blogu yake hapa. Pia kuna mahojiano yake hapa. Anajihusisha na mradi wa world changing. Kongoli hapa. Na mkono wake uko nyuma ya mradi huu hapa.
Mon 18 Apr 2005
Mon 18 Apr 2005
Moja ya mabadiliko makubwa yanayotokana na teknolojia ya zana mpya za habari za mawasiliano na habari ni uwezo wa wananchi wenye nyenzo hizi kuweza kupata habari kwa urahisi zaidi na pia kushiriki katika mijadala ya kisiasa. Mfano mmojawapo ni tovuti ya uchaguzi Tanzania iliyoko hapa.
Mon 18 Apr 2005



