Nakiri kuwa sio rahisi kuukacha mtandao. Ingawa jana nilisema kuwa huenda tukaonana wiki ijayo, nimeshindwa kujizuia kuja kuchungulia blogu kadhaa na kuandika. Kuna mradi ambao ningependa kuutangaza (ninaupigia debe maana ninahusika nao). Jana nimepata makaratasi toka kwa mwanasheria wa mradi wa The People Yes, Jordan wa Smith Moore Law. Mimi ni mmoja wa wakurugenzi wa mradi huu ambao moja ya madhumuni yake ni kutoa nafasi kwa watu wanaoitwa “watu wa kawaida” kuweza kutoa maoni yao, kujielezea, n.k. Mradi huu ni moja ya miradi ambayo inaingia kwenye kundi la miradi ya Uandishi wa Wananchi.
May 2006
Fri 26 May 2006
Thu 25 May 2006
Wikiendi hii, mikutano mwezi ujao…
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: mseto , Mengineyo , mikutanoToa Maoni [9]
Kwakuwa mama Ukweli anahitimu digrii yake ya pili jumamosi ya wiki hii toka katika chuo kikuu cha School for International Training, huenda nisiweze kuandika chochote hadi wiki ijayo. Ninaondoka leo usiku kwenda Vermont ambapo ndipo kilipo chuo cha School for International Training. Huenda nikapata muda wa kuingia mtandaoni, au nisipate. Wapo marafiki wengi wa kutembelea na kupiga nao soga kule Vermont hivyo mtandao naweza niupe kisogo. Kwa mfano, yupo ndugu yangu toka Morocco, Mokhtar Bouba, ambaye baada ya kumpigia kelele sana niliweza kumshawishi aanze kublogu kwa lugha yake, Kitamazight. Blogu yake hii hapa.
Tue 23 May 2006
Kwanini Bloglines na Co.mments ni zana muhimu kwa Afrika?
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: wanablogu , zanaToa Maoni [9]
Kabla sijazungumzia mada iliyonifanya nikae chini kuandika, napenda kueleza furaha yangu kwa mfumuko wa wanablogu unaondelea kila siku. Mwandani anatupasha kuwa Simon Kitururu kakata shauri. Hii ni habari njema sana maana Simon amekuwa ni kati ya Watanzania ambao wamekuwa wakitupa tafu wanablogu kwa muda mrefu. Amekuwa msomaji wa blogu zetu toka zamani. Sasa naye ameamua kujimwaga uwanjani. Mtazame hapa. Wakati namtembelea Simon, mara nakutana na blogu nyingine ya Watanzania walioko Norway. Bonyeza hapa uione. Huenda huu ni mwanzo wa kuwa na blogu za makundi kama ilivyo blogu ya ndugu zetu walioko Norway.
Mon 22 May 2006
Dada Miriam na blogu ya mapishi kajimwaga uwanjani…
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: wanabloguToa Maoni [2]
Aje hapa tuhangaike naye…
Huyo ni dada Miriam ambaye nilimzungumzia majuzi (soma hapa). Anasema kuwa wanablogu wa Tanzania tunazumgumzia karibu kila kitu ila tumesahau kitu kimoja: maakuli. Kaanzisha blogu ya mapishi. Mtembelee, mkaribishe. Na pia jifunze mambo kadhaa kuhusu mapishi ya Kitanzania. Bonyeza hapa. Pamoja na blogu, Miriam ana tovuti pia. Bonyeza hapa.
Blogu yake itakuwa ya Kiswahili na kiingereza.
Tue 16 May 2006
Unataka kurusha matangazo ya redio bila kuwa na kituo cha redio?
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: zana , podikasitiToa Maoni [30]
Hivi karibuni nimeanza kujihusisha na vuguvugu la kuwezesha watu wa kawaida kama mimi na wewe kuweza kuwa na kituo cha redio chumbani kwako ili urushe matangazo redioni! Tofauti na teknolojia kama ya podikasti, ambayo inakuwezesha kurusha matangazo kwenye Intaneti, teknolojia hii inakuwezesha kurusha matangazo toka kwenye Intaneti kwenda kwenye redio. Vuguvugu hili linaitwa Broadcast Your Podcast (BYP). BYP inawezesha wanablogu wa sauti (wanablogu wasiotumia maandishi bali sauti) kutuma matangazo yao sio tu kwenye Intaneti au zana za kusikiliza mafaili ya mp3 (vitu kama iPod) bali pia kwenye redio kupitia mitabendi za masafa mafupi, FM.
Sat 13 May 2006
Mwanablogu mwingine wa Kiswahili toka Kenya. Huyu ni ndugu Mari-Djata Amadi ambaye niliwahi kumzungumzia huko nyuma. Bonyeza hapa usome niliyoandika. Najua blogu yake itakuwa changamoto kwetu Waafrika. Ukitembelea utaona kuwa Amadi anatumia lugha kwa ufundi mkubwa (ingawa anatoka nchi ambayo huwa wakati mwingine tunadhani kuwa hawajui Kiswahili. Blogu zinatudhihirishia kuwa wako wanaoifahamu lugha hii nchini humo). Anataka tujisaili. Bonyeza hapa umsome na kumkaribisha. Karibu sana.
Sat 13 May 2006
Kama huifahamu blogu ya Bongo Kijiweni, basi bonyeza hapa.
Sat 13 May 2006
Kituo cha Mafuta! (nimeibadili kidogo video niliyoiweka jana)
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: videoToa Maoni [1]

Bonyeza hapa (au juu ya picha hapo juu) utazame video.
Kuna Marikani na Marikani. Kuna Marikani ya filamu za Hollywood na majarida kama Ebony. Na kuna Marikani ambayo watu wengi hatuijui. Na wengine waliijua baada ya maafa ya Katrina. Kuna Marikani ya vituo vya mafuta “mshenzi” na vyuo vikuu vya vinyonzi
Sat 13 May 2006
Kuna wanablogu ambao huwa wakijitokeza nafsi yangu hutulia maana ninakuwa nimewasubiri kwa muda mrefu. Mvumilivu hula mbivu. Yuko dada yetu ninayemsubiri. Nina subira. Lakini wakati tunamsubiri, ningependa utembelee tovuti yake. Tovuti hii ni nzuri sana kwa wale wapenda maakuli. Wanaopenda kupika (Jeff na Boniphace mnapika au mnakula vyakula vya papo kwa hapo? Nambiza, bado unapenda pilipili?). Huyu ni dada yetu Miriam ambaye pamoja na mambo mengine ni mtaalamu wa mapishi ya Kitanzania. Bonyeza hapa upate masomo ya mapishi.
Tue 9 May 2006
Rafiki yangu Babukadja Sankofa ametoa maoni baada ya Jikomboe kuingia katika hatua nyingine ya kuwa videoblogu. Babukakadja ni mtengeneza filamu. Teknolojia hii ya videoblogu ni muhimu sana kwa watu kama yeye. Katika maoni yake, ambayo nitayaweka hapa, ameongelea jambo ambalo ndio msingi wa kitabu kilichoandikwa na mwanasafu wa gazeti la New York Times, Thomas Friedman. Yeyote ambaye kwa njia moja au nyingine anaweza kukipata kitabu hiki na kukisoma, tafadhali fanya hivyo. Kitabu chenyewe kinaitwa The World Is Flat. Yaani Thomas Friedman anasema kuwa dunia sio duara tena. Dunia, siku hizi, ni tambarare! Galileo aliposema dunia ni duara aliadhibiwa vikali na kanisa katoliki la Rumi. Leo hii Friedman anatuambia dunia ni tambarare…
Sun 7 May 2006
Bonyeza hapa (au hapo juu kwenye video) ili utazame.
Nimekuwa nikifuatilia masuala ya kublogu kwa video kwa muda mrefu. Kutokana na kuwa nimekuwa na uzoefu wa kujielezea, kutoa maoni, na habari kwa maandishi, imenichukua muda mrefu kuamua kama ninapenda kutumia sio tu maandishi bali pia video kufikisha ujumbe. Baada ya kutazama masuala ya kublogu kwa video kwa undani nimegundua kuwa kila njia ya kufikisha ujumbe ina nafasi yake. Kuna mambo ambayo ukitumia maandishi ujumbe unafika, lakini mambo mengine ujumbe unakuwa mkavu. Kwa mfano, video ya kwanza niliyoipandisha leo. Ningeamua kuelezea unayoona kwenye video hiyo kwa maandishi tu ujumbe usingefika jinsi ninavyotaka.
Sun 7 May 2006
Kuna jambo moja kubwa na zuri sana linajitokeza katika blogu zetu. Jambo hili ni kati ya mambo ambayo hunifanya nione kuwa kazi tunayofanya katika kujenga kijiji chetu hiki sio ya bure.
Tumezoea kusema kuwa blogu zetu hizi ni kisima cha maarifa. Pengine wakati mwingine huwa hatutoi mifano ya kuonyesha jinsi gani ilivyo kisima cha maarifa. Huenda pia tunapoita jamii yetu hii kuwa ni kijiji, baadhi yetu au wasomaji wetu wanaweza wasielewe kwanini tunaita kijiji.
Sun 7 May 2006
Kumbe inawezekana kwa mahakama zetu kuwa kimbilio la watu wanaotaka kuboreshwa kwa mfumo wa demokrasia nchini Tanzania? Majuzi mahakama kuu ilifuta sheria chafu inayosafisha njia kwa matajiri kuchukua nafasi za uongozi na masikini kuwa ni wapiga kura, waandamanaji, washabiki, wavaa fulana, na wasukuma magari yao. Bonyeza hapa usome juu ya kufutwa kwa sheria chafu ya takrima. Sasa mahakama hiyo hiyo imetoa uamuzi mwingine mzito.
Fri 5 May 2006
Ule mkutano mkubwa wa We Media nilioandika juu yake (bonyeza hapa usome iwapo hukusoma niliyoandika) ulikuwa na mjadala kuhusu Afrika ambapo kati ya washiriki ni mwanablogu Ory Okollah (aliyeshiriki akiwa Afika Kusini [mambo ya teknolojia hayo]). Soma mjadala huo kwa kubonyeza hapa.
Wed 3 May 2006
Nilikuwa natafuta mambo fulani niliyoandika zamani. Katika tafutatafuta nikakuta porojo hii niliyoandika mwezi wa pili mwaka jana. Pengine hukuisoma. Isome sasa…
——
Nakumbuka ile siku nilipofika Chicago kwa mara ya kwanza. Miaka miwili iliyopita. Sikupapenda hata kidogo. Mbio sana. Shimeshime. Utu hakuna. Hakuna wa kumsimamisha kumuuliza saa.
Chicago kuna kila kitu. Kuna utajiri uliokithiri na kuna ufukara unaokutoa machozi. Kuna baadhi ya mitaa ukifika unajiona kama uko sokoni Kariakoo. Tena kule shimoni. Na mingine ukienda lazima uwe na roho ya paka. Silaha nje nje. Vibaka kama utitiri. Michoro ya majina na alama za magenge kila ukuta. Milio ya ving’ora vya polisi na risasi kila saa.
Wed 3 May 2006
Tafadhali fuatilia mkutano mkubwa kuhusu teknolojia na nyanja ya habari nchini Uingereza. Mkutano huu, We Media, ni wa pili kufuatia ule wa kwanza uliofanyika New York (ambao nilihudhuria).
Mkutano huu unakutanisha wanablogu, maripota, wakurugenzi wa vyombo vya habari na makampuni ya teknolojia, wahariri, watafiti, n.k. Ingawa mkutano wenyewe unafanyika Uingereza tarehe 3-4 mwezi huu, unaweza kushiriki. Hivi ndivyo teknolojia mpya za habari zinavyobadili mambo na kutuwezesha kufanya mambo ambayo huko nyuma tulikuwa hatuwezi kufanya. Unaweza “kuhudhuria” kwa njia kadhaa. Bonyeza hapa uweze kusikiliza, bonyeza hapa utazame video moja kwa moja, bonyeza hapa ushiriki kwenye majadiliano na watu wengine wanaohudhuria mkutano huu. Bonyeza hapa utazame programu nzima ili uweze kuamua unataka kushiriki kwenye mjadala gani. Mimi nitashiriki mkutano mzima kama vile niko kwa Malikia Lizabeti. Yapo mambo mengi ya kujifunza iwapo unakereketwa na teknolojia mpya za habari, mawasiliano, na maarifa. Sijui wewe.
Tue 2 May 2006
Kiswahili Umoja wa Mataifa (au umoja wa Marekani na marafiki zake?)
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: lughaToa Maoni [6]
Wakati tunapata habari kuwa kiingereza sio lugha kuu bloguni, Maitha anatupa habari kuwa Koigi Wamwere ameanzisha kampeni Umoja wa Mataifa (mwanamuziki Fela Kuti alikuwa akiita umoja huu, “Dis-United United Nations”!) kutaka Kiswahili kutambuliwa kama lugha rasmi ya umoja huo. Ingawa Kenya huchukuliwa kuwa haitilii maanani Kiswahili, nchi hiyo imefanya jambo muhimu sana la kutaka lugha hii kupewa hadhi ya juu. Tunapozungumzia Kiswahili fahamu kuwa tunazungumzia lugha inayozungumzwa na watu zaidi ya milioni 100.
Mon 1 May 2006
Kiingereza sio lugha kuu au ya msingi katika ulimwengu wa blogu. Lugha ya kwanza ni ipi? Bonyeza hapa umsome David Sifry akizungumzia ukuaji wa blogu, lugha, na matumizi ya maneno kuashiria maudhui (tagging).



