Anousheh Ansari sio tu mwanamke wa kwanza kuwa mtalii katika anga za mbali, bali pia ni mwanablogu wa kwanza kublogu akiwa nje ya dunia yetu! Blogu hadi huko angani, nje ya dunia. Bonyeza hapa usome blogu yake aliyokuwa akiandika kuhusu safari yake hiyo.
September 2006
Sat 30 Sep 2006
Thu 28 Sep 2006
Maggid Mjengwa + Dis-United United Nations!
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: wanablogu , global voicesToa Maoni [7]
Hivi ulidhani kuwa Maggid Mjengwa hataki kublogu? Hebu acha utani…bonyeza hapa. Karibu sana Maggid!
——
Huko nyuma niliandika kuhusu mahojiano yaliyofanywa na shirika la habari la Uingereza, Reuters na yule jamaa aliyetoa mamilioni mengi kwa ajili ya “Dis-United United Nations” (yaani Umoja wa Mataifa), Ted Turner. Bonyeza hapa usome niliyoandika kuhusu tukio hilo, kisha bonyeza hapa usome aliyoandika Rebecca MacKinnon kuhusu mahojiano hayo.
Mon 25 Sep 2006
Balaa la Digital Indaba - 4 na Mkutano wa Wanablogu wa Afrika- 2007
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , wanablogu , mikutanoToa Maoni [2]
Nimeandika muhtasari wa kiingereza kuhusu ule mjadala mkali kuhusu mkutano ulioitwa the Digital Citizen Indaba on Blogging. Niliandika kuhuzu mzozo huu katika makala fupi zenye sehemu tatu. Bonyeza hapa usome sehemu ya kwanza, hapa kwa sehemu ya pili, na hapa ni sehemu ya tatu. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
Sun 24 Sep 2006
DarHotwire: Tafadhali, Msitumie Kazi za Wanablogu Bila Idhini!
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , sheriaToa Maoni [11]
Moja ya nyanja ambazo zinapata changamoto kubwa kutokana na mabadiliko ya kasi ya teknolojia ni nyanja ya sheria. Teknolojia zinabadilika na kuimarika kila siku na katika kufanya hivyo zinabadili nyanja za uchumi, siasa, habari, elimu, burudani, na utamaduni. Ni jinsi gani ambavyo watunga sheria wataweza kuhakikisha kuwa kunakuwapo na sheria ambazo zinakidhi mahitaji ya wakati?
Kesi iliyoihusu kampuni ya Yahoo! (bonyeza hapa na hapa) ni moja ya vielelezo vya changamoto ninayozungumzia.
Hata hivyo, pamoja na mabadiliko ya kasi ya teknolojia, misingi ya sheria nyingi bado iko pale pale. Kwa mfano, sheria ya hakimiliki. Bado ni kosa kisheria na pia sio ustaarabu kuiba kazi za mtu mwingine (iwe ni maandishi, picha, filamu, muziki, n.k.) bila idhini ya mtu huyo. Hata kama kazi hizo ziko ndani ya blogu. Ndio, hata kama kazi hizo ziko ndani ya blogu. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
Tue 19 Sep 2006
UN: Will They Listen? Fela anaweza kutupa jibu…
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: demokrasia , global voicesToa Maoni [12]
Leo saa kumi jioni kutakuwa na majadiliano kuhusu mageuzi ndani ya Umoja wa Mataifa (au kwa jina jingine: Umoja wa Marekani na wenzake wachache). Mahojiano hayo yataendeshwa na mhariri wa masuala ya siasa wa shirika la habari la Uingereza, Reuters, Paul Holmes. Holmes atakuwa akimhoji Ted Turner, mwanzilishi wa shirika kubwa la uongo duniani la CNN. Karibu miaka kumi iliyopita Ted Turner alitoa dola bilioni moja kwa ajili ya kusaidia Umoja wa Mataifa. Mahojiano hayo, au tuseme mazungumzo hayo yatahusu miaka kumi baada ya mchango wake huo (hakuna mtu binafsi ambaye amewahi kutoa fedha nyingi kiasi hiki kwa Umoja wa Mataifa) na mambo mengine yanayohusu vyombo vya habari. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii). (more…)
Mon 18 Sep 2006
Mradi wa Global Voices wapata tuzo!
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: mseto , blogu , global voicesToa Maoni
Ni furaha iliyoje kwa wanablogu wanaojihusisha au kufaidika na kazi za mradi wa Global Voices. Mradi huu umepata tuzo kubwa kwa ubunifu na utendaji kazi mahiri. Tuzo hiyo ya the Knight-Batten Awards for Innovations in Journalism ilikuwa ikigombewa pia na jamaa wengine sita. Bonyeza hapa utaona orodha ya jamaa hao wengine na pia ukishuka chini kabisa utaona washindi wa mwaka jana. Mradi huu ambao bado ni mbichi kabisa ulishinda huko nyuma tuzo ya Best of Blogs, bonyeza hapa kama ulipitiwa.
Mon 18 Sep 2006
Tafadhali jibu maswali kuhusu Mradi wa Global Voices
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , global voicesToa Maoni
Iwapo wewe ni msomaji wa blogu ya mradi wa Global Voices (kama wewe sio msomaji basi utafute muda uwe unaisoma), tafadhali chukua dakika chache ujibu maswali ambayo yatasaidia kuboresha mradi huu. Bonyeza hapa usome namna ya kushiriki kujibu maswali hayo. Fomu yenyewe yenye maswali utaipata ukibonyeza hapa. Lakini ni vyema ukasome kwanza yaliyoandikwa kwenye kiungo hiki kabla ya kujibu maswali yenyewe.
Sat 16 Sep 2006
Leo ni Software Freedom Day duniani. Afrika hatuko nyuma katika kukumbuka siku hii. Bonyeza hapa usome yanayotokea Afrika kwa ajili ya hii siku. (Anna Dani: daima mbele!)
Sat 16 Sep 2006
Rafiki yangu mpendwa, Yvonne Ndege wa BBC, amefanya mahojiano na yule bwana aliyechezea moto nchini Kenya kwa kutaka kufichua wezi halisi (Wezi halisi ni tofauti na wale wezi wa shilingi elfu 20 au elfu 50 ambao huitwa vibaka. Wezi halisi ni wale wezi wa mabilioni ambao huitwa “viongozi” na hupewa cheo cha “waheshimiwa.”). Huyu ni ndugu John Githongo, ambaye baada ya kupeleka macho yake kusikotakiwa ilimbidi aondoke Kenya na kukimbilia Uingereza. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
Thu 14 Sep 2006
Skolashipu za kuhudhuria “TEDGlobal” jijini Arusha, Tanzania
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: mseto , skolashipu , mikutanoToa Maoni [6]
Ule mkutano wa kila mwaka wa masuala ya teknolojia, TED (technology, entertaiment, design) unaandaa mkutano mkubwa barani Afrika kwa mara ya kwanza. Mkutano huo uliopewa jina la TEDGlobal: Africa the next chapter, utafanyika Juni 4-7 Arusha (au “Arusa”) nchini Tanzania. Zipo skolashipu 100 hasa kwa wahudhuriaji walioko Afrika. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii na ukishamaliza tuma maombi yako bila kuchelewa. Wakikutalia niambia niwaonyeshe kilichomnyoa nanii hii, nini hii!).
Thu 14 Sep 2006
Digital Indaba imeleta balaa - 3
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , wanablogu , mikutanoToa Maoni [3]
Ule mjadala mkali kuhusu wanaohudhuria na walioalikwa kwenye mkutano wa Digital Citizen Indaba unaendelea. Niliandika kuhusu mjadala huu mkali kiasi cha kutoa cheche za moto katika sehemu mbili. Bofya hapa usome sehemu ya kwanza na hapa usome sehemu ya pili. Usiache kusoma maoni ya wasomaji katika blogu ninazokupa zenye mjadala huo.
Thu 14 Sep 2006
Waandishi wa habari: tuma maombi mapema!
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: waandishi wa habari , nafasi za kaziToa Maoni [3]
Iwapo wewe ni mwandishi wa habari na ungependa kufanya kazi (kwa muda mfupi) katika mradi uitwao Knight International Press Fellowships kama “journalism fellow,” basi tuma maombi mapema. Tarehe ya mwisho watuma waombi wanaotoka nje ya Marekani ni Oktoba 10, 2006. Maelezo kamili utayapata katika tovuti yao kwa kubinya hapa. Maelezo yako ukurasa wa mbele.
Wed 13 Sep 2006
Digital Indaba imeleta balaa - 2
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , wanablogu , afrika , mikutanoToa Maoni [2]
NYONGEZA: (kabla ya kusoma hii hakikisha umesoma niliyoandika jana kwa kubinya hapa. Hii ni nyongeza ya hiyo ya jana, kwa maneno mengine, “sehemu ya pili”).
(muhimu sana sana usome maoni katika viungo hivyo nilivyokupa hapo chini)
Mjadala bado unaendelea. Kila upande unarusha kete zake. Ningependa usome kwa makini maoni aliyotoa Kenyan Pundit ambayo ni changamoto kwa Waafrika. Anasema:
(tongue firmly in cheek, and wake me up as soon as “true” Africans plan, fund, and organize, the “true” African blogging indab…um..meet-up)
Maana yake, kwa tafsiri yangu ambayo sio ya moja kwa moja, anasema, Waafrika wanaojiita Waafrika halisi (maana Waafrikana, wazungu wa Afrika Kusini wametolewa kwenye kundi hilo la Waafrika na baadhi ya wachangiaji wa mjadala), wanasubiri nini wasiandae mkutano wao? Kwani lazima wakaribishwe?
Haya, kuendeleza mjadala yupo yule mwanablogu ambaye wanablogu wa Kenya hupenda kumuita “baba” wa blogu za Kenya, Mental Acrobatics. Ameingilia mjadala huu kwa staili ya aina yake. Yeye anasema mzozo mkubwa sio kuhusu waalikwa...bonyeza hapa usome. Halafu, Ethan Zuckerman naye ameamua kutoa ufafanuzi zaidi kuhusu mkutano huu. Bonyeza hapa. Pia Sokari Ekine hajabaki nyuma. Anasema: White Blogging Africa. Msome hapa.
Tue 12 Sep 2006
Digital Indaba imeleta balaa kama Mesenja…1
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , wanablogu , mikutanoToa Maoni [16]
Unakumbuka wimbo wa “Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa meneja”?
Ule mkutano nilioutangaza siku za nyuma (bonyeza hapa) uitwao “Digital Citizen Indaba” ulio chini ya mkutano wa kila mwaka wa Highway Africa umezua kasheshe katika ulimwengu wa blogu. Hii “indaba” ni indaba kweli au ni indaba babaisha? Ndio wanauliza baadhi ya wanablogu na watoa maoni. Mwanablogu Bullets and Honey alianza kuhoji mkutano huu kama ni wanablogu wa Afrika au ni indaba ya wazungu na waafrika wachache. Akaandika makala aliyoiita: (White?) African Blogger Conference in a Week. Isome hapa utazame na mjadala mkali kwenye sehemu ya maoni. Kisha Vincent Maher, mmoja wa waandaaji akajibu. Akasema kuwa alichoandika Bullets and Honey ni ubaguzi wa rangi. Msome hapa. Bullets and Honey anamwita Vincent Maher, Vincent “Madiba” Maher. Hiyo ni kejeli na sio kumsifia.(bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
Sun 10 Sep 2006
Mwidimi Ndosi ni rafiki yangu wa siku nyingi sana. Nakumbuka nikiwa kidato cha kwanza/pili pale Mawezi sekondari, Moshi, miaka hiyo. Enzi zile za Mwalimu Sango na yule mwalimu wa hisabati, Mashingia, aliyeniambia, “Chijana mwandiko wako tu unaonyesha kuwa hesabu zinakupiga chenga.” Mashingia: hukuwa umekosea. Basi Mwidimi na wenzake ni kati ya watu walionitia hamasa ya kujifunza gitaa kwa bidii. Walikuwa wakinikuna sana. Nakumbuka nikienda pale kwenye ofisi ya Ukwata (sikumbuki vizuri…nadhani ilikuwa ni ofisi ya Ukwata) walipokuwa wakikutana Mwidimi, Ibrahim, Mboneke na pia Dunstan. Wanakutaka pale, wanakung’uta magitaa. Nyuzi bin nyuzi. Mimi natazama tu. Na wakati mwingine kugusagusa huku vidole vikishikwa na kigugumizi. (Mwidimi: siku hizi nakwambia hunitoi! Tutatoana jasho. Au unabisha? Iwe blues, jazz, za Kiafrika kama zile za Kizaiko Langalanga, au kama za Ali Farka Toure, changanya zote). (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
Sat 9 Sep 2006
Wasomaji wakichukua kazi ya mhariri itakuwaje?: Zoezi la Wired News
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: teknolojia , Uandishi wa Raia , Mengineyo , wikipediaToa Maoni
Siku moja niliandika kuhusu teknolojia ambazo zinawezesha wasomaji kuwa “wahariri” kwa kuweza kuamua habari zipi zikae ukurasa wa mbele, wajibu ambao kawaida huwa ni wa mhariri. Nikauliza, “hivi mhariri mkuu ni nani vile?” Nilisema kuwa hadhira, yaani wasomaji, wasikilizaji, na watazamaji wana jina jipya, wanaitwa (kwa kiingereza): People formerly known as audience. Bonyeza hapa usome niliyoandika siku hiyo. Sasa katika kuendeleza jambo nililozungumzia siku hiyo, yaani teknolojia zinazobadili uhusiano kati ya vyombo vya habari na hadhira, leo ninakupa mfano mwingine. Mfano huu ni tofauti kidogo na ule wa wasomaji kuwa na uwezo wa kuamua habari zipi ziwe ukurasa wa mbele. (bonyeza hapo chini umaliza kusoma habari hii).
Sat 9 Sep 2006
Shirika la Dropping Knowlege limefanya jaribio la aina yake. Limekusanya maelfu ya maswali toka kwa watu mbalimbali duniani kupitia tovuti yake. Kisha likachagua maswali 100. Likachagua watu 112. Likawakutanisha katika meza moja kubwa katika eneo ambalo serikali ya Kinazi huko Ujerumani ilichoma moto vitabu. Watu hao wakaulizwa maswali hayo 100, wakayajibu kwa wakati mmoja, kila mmoja akiwa anarekodiwa. Nenda hapa usikilize mwenyewe wakijibu maswali hayo na kujua zaidi kuhusu mradi huu.
Fri 8 Sep 2006
Marastafari: Kwenye rege wapo na kwenye blogu wapo!
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: blogu , wanabloguToa Maoni
Marasta nao kwanini wasiblogu? Tazama hapa. Karibu Luihamu. Irie! Jah, rastafari!
Wed 6 Sep 2006
Hadi Masama Rundagai kule mkoani Kilimanjaro wanataka nao kusema yao kupitia teknolojia ya blogu. Fuatilia ya Rundugai kwa kubonyeza hapa.
Wed 6 Sep 2006
Washiriki wa mjadala kuhusu lugha za Afrika BBC
Na Ndesanjo Macha, Maudhui: utamaduni , lugha , wikipedia , afrikaToa Maoni [2]
Ule mjadala kuhusu Wikipedia na lugha za Kiafrika ni leo. Bonyeza hapa usome nilipoutangaza jana (kumbuka unaweza kuusikiliza redioni au mtandaoni kwa kutazama kubonyeza pale pasemapo “Listen to the programme” katika kiungo hiki). Nitashiriki kwenye mjadala huo pamoja na watu wengine kama ndugu Martin Benjamín wa mhariri wa Kamusi Hai ya Kiswahili Kwenye Mtandao, Kasper Souren, mwanzilishi wa Wikipedia ya Kibambara, Tido Mhando, mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, na wengineo. Pia unaweza kutazama mjadala uliofanyika mtandaoni kuhusu umuhimu wa lugha za Afrika kwa kubonyeza hapa.



