November 2006
Monthly Archive
Fri 24 Nov 2006
SAMAHANI BLOGU HII ILIPOTEA KIDOGO BILA TAARIFA. kULIKUWA NA UKARABATI KIDOGO. SASA IMERUDI.
—
Simon Kitururu wa Chakula cha Mawazo ameanza kusukuma gurudumu la kujenga jumuiya yetu. Ametoa mawazo yake juu ya mambo ambayo hayakutolewa maamuzi siku ile ya mkutano wa wanablogu wa Tanzania. Pamoja na kuwa wana kamati itabidi wawasiliane na kila mwanablogu, utaratibu huu aliouanzisha Kitururu wa kutumia blogu yake kuchangia katika mjadala kuhusu jumuiya yetu ni mzuri. Ninaamini kuwa wanablogu wengine wenye nia ya kujumuika kujenga jumuiya rasmi ya wanablogu wa Tanzania watatumia blogu zao kujadili masuala ambayo tunatakiwa kuyapatia ufumbuzi. (bonyeza hapo chini umalize kusoma)
(more…)
Thu 23 Nov 2006
Na Ndesanjo Macha, Maudhui:
skolashipuToa Maoni [2]
Huenda usiwe na muda wa kutosha kufuatilia habari hii maana mwisho wa maombi ni Desemba 1 (kama nimeelewa ujumbe vizuri). Hizi ni nafasi za kusoma nchini Norway. Bonyeza hapa usome ujumbe kuhusu nafasi hizo toka kwa ndugu Kweka. Ukiwa na maswali zaidi unaweza kuwasiliana naye kupitia anuani hii: ekweka2001@yahoo.co.uk
Thu 23 Nov 2006
Na Ndesanjo Macha, Maudhui:
teknolojia ,
afrika ,
zanaToa Maoni [1]
Jamaa wa Geekcorps jamani…kwanza walikuja na antena kwa ajili ya mtandao usiwaya (WiFi) inayotengenezwa kwa kutumia chupa za maji kule Mali. Sasa wamekuja na mradi wanauita “Luninga ya Kopo” (CanTV). Yaani wanatumia makopo kutengeneza antenna ambazo wanavijiji wanatumia kupata matangazo ya luninga! Bonyeza hapa usome habari hii niliyoiandika katika blogu ya Pop!Tech.
Mon 20 Nov 2006
**Usisahau kumpigia Jeff kura. Leo ni mwisho wa raundi ya kwanza. Bonyeza hapa. Matokeo ya mchuano ni haya.
———–
Maneno hayo hapo chini toka kwa msimamizi wa mkutano, Msangi Mdogo, ndio yaliyofungua mkutano wetu rasmi:
NA SASA NAFUNGUA KIKAO RASMI KWA KUWAKARIBISHA NYOTE MLIOBAHATIKA KUHUDHURIA MKUTANO HUU WA KWANZA NA WA AINA YAKE KATIKA HISTORIA YA NCHI YETU. KWA WALE WALIOKO NYUMBANI TANZANIA ULIPEWA NAFASI KIDOGO KATIKA GAZETI LA MAJIRA LEO
KUNA DAKIKA MBILI KABLA YA MKUTANO KUANZA RASMI, NAOMBA TUJIPANGE KWENYE NAFASI ZETU TAYARI KWA MKUTANO
Baada ya hapo mkutano ulianza na kuendelea vyema hadi mwisho. Kuna wajumbe ambao walipata tatizo la kuingia ukumbini, nawapa pole. Naamini mkutano ujao utaboreshwa zaidi. Shukrani zimwendelee ndugu Mike Mushi “Mzee wa Mlango wa Uani” ambaye aliweza kubomoa ukuta na kuweka mlango wa uani uliowawezesha wajumbe waliokuwa na matatizo ya kuingia waweze kuingia kupitia mlango huo. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii)
(more…)
Sun 19 Nov 2006
Kichwa cha habari hapo juu ni kichwa cha makala niliyoandika kuhusu mkutano wetu (ambao nikiufikiria ninasisimka) ambayo imetoka leo kwenye gazeti la Mwananchi. Wiki ijayo nitaandika kwenye gazeti hilo mambo ya msingi yaliyoamuliwa. Ninapitia mkutano mzima ili niweze kutoa muhtasari wake kwenu nyote. Bonyeza hapa usome makala hiyo. Habari za mkutano wetu zimeandikwa pia kwenye ukurasa wa Global Voices Online. Shukrani Nambiza Tungaraza kwa kuandika habari hiyo. Bonyeza hapa uisome.
Sun 19 Nov 2006
Na Ndesanjo Macha, Maudhui:
teknolojia ,
bloguToa Maoni
Gazeti la The Economist lina habari kuhusu wanablogu walioacha kazi na hivi sasa blogu zao ndio zinawaingizia mkono kinywani. **Usije ukaacha kazi baada ya kusoma habari hii!**
Utaona mmoja wao anasema kuwa ilimchukua miaka mitano ya kukesha hadi kufikia hatua ya kutumia blogu yake kupata kipato. Bonyeza hapa usome habari hii. (bonyeza hapo chini uendelee kusoma)
(more…)
Sat 18 Nov 2006
Mkutano ndio umemalizika. Wanaondoka wajumbe mmoja mmoja. Wengine wamebaki kwenye mazungumzo baada ya kikao. Baadhi ya wajumbe walipata matatizo kuingia ukumbini. Nawapa pole. Wakati mwingine tutajitahidi kufanikisha zaidi. Asante Mushi kwa kuokoa jahazi na kuwezesha waliokuwa na matatizo kuingia ukumbini. Muhtasari wa yaliyoongelewa na kukubaliwa utaupata. Ni furaha ilioje. Asanteni wote mliohudhuria.
Sat 18 Nov 2006
Ukumbi wa mkutano umeanza kuwa kama ukumbi wa mkutano. Gumzo kabla ya habari linaendelea. Nilitaka kusema mawili matatu. Ningependa sana tutumie muda wetu vyema. Hivyo kila mshiriki ajitahidi kuwa ndani ya mada. Kwa baadhi yetu hili linaweza kuwa jambo gumu. Tujitahidi sana kuwa ndani ya mada.
Tafadhali unapoingia ndani ya mkutano tumia jina lako ili tufahamu wewe ni nani. Inawezekana ukatoa wazo ambalo linahitaji kufanyiwa kazi. Hivyo tukahitaji kukufuata kujua “nyuma” unayotaka tujenge iwe ni ya mabati au vigae. Kama ni vigae, viwe vya rangi gani? Au tuezeke nyasi? Kwahiyo kuna umuhimu wa kufahamu nani anasema nini.
Iwapo wewe hujulikani kwa wanablogu, basi jitambulishe wakati wa kuingia. Unaweza kusema, “Mimi ni fulani bin fulani. Ni msomaji wa blogu.” Au, “Mimi ni fulani fulani, ninataka kuanza kublogu.” Kitu kama hicho.
Unaposhiriki, jua kuwa kila kitakachosemwa kitahifadhiwa na baadhi ya wanablogu wanaweza kuweka kwenye blogu zao. Iwapo unasema jambo ambalo hungependa lihifadhiwe, na una sababu za msingi, basi sema hivyo.
Naamini kuwa tutaendesha mkutano kwa heshima na busara. Bonyeza hapa kuingia ukumbini.
Sat 18 Nov 2006
Yanakaribia kuwa! Ninavyoandika sentensi hizi, tayari kuna watu ukumbini. Nimekutana pale na ndugu Mike Mushi wa Habari Tanzania na Richard Mushi wa blogu hii hapa. Tayari kamkutano fulani fulani hivi kameanza. Usishtuke. Saa ya mkutano bado. Ni gumzo za hapa na pale. Mazungumzo kabla ya habari. Kama hujui nazungumzia mkutano gani. Bonyeza hapa.
Nitaandika tena kabla ya mkutano…usiondoke. Kuna mambo mawili matatu muhimu.
Fri 17 Nov 2006
Wakati tunahesabu masaa kabla ya ule mkutano wetu wa wanablogu na wapenzi wa blogu wa Tanzania, nimepata habari njema zinazohusu blogu ya mwenzetu. Blogu ya kimombo ya Jeff Msangi imeteuliwa katika kinyang’anyiro cha tuzo za blogu bora nchini Kanada (2006 Canadian Blog Award). Blogu hiyo, African Perpective, iko katika kundi la blogu bora za Kitamaduni (Best Cultural Blog). Bonyeza hapa umpigie kura (shuka chini kwenye orodha ya “best cultural blog). Bonyeza hapa usome blogu yake ya African Perpective.
Haya, mkutano wetu ndio huo. Kuna maelezo ya hatua kwa hatua ya jinsi ya kuingia kwenye chumba cha mkutano. Maelezo hayo yako kwenye ukurasa maalum wa wiki wa mkutano wetu. Bonyeza hapa. Tafadhali sana fuata maelezo hayo hatua kwa hatua, la sivyo utabaki nje ya ukumbi ukipiga soga na wapita njia. Kwa taarifa yako kutakuwa na chai, kalimati, sambusa, vitumbua, kashata na mapochopocho mengine ya Kitanzania kwa hisani ya Miriam! Shauri yako! (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii)
(more…)
Tue 14 Nov 2006
Kura zimepigwa kutafuta saa ya mkutano wa wanablogu na wapenzi wa blogu wa Tanzania. Mkutano utafanyika saa nane mchana saa za Tanzania, Novemba 18, 2006. Wapiga kura waliochagua saa nane mchana wameshinda. Hakuna masanduku ya kura yaliyoibwa wala kura zilizoharibika. Wala hakuna pingamizi lolote. Mrema angeshiriki pengine tungekuwa tunaelekea mahakamani hivi sasa! Maandalizi ya mkutano yanaendelea katika ukurasa wa wiki ambao utaupata kwa kubonyeza hapa. Tafadhali shiriki kwenye maandalizi. Ukipata tatizo la jinsi ya kuweka maoni yako kwenye ukurasa wa maandalizi ya mkutano, bonyeza hapa usome maelezo mafupi. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii)
(more…)
Sun 12 Nov 2006
Leo ndio mwisho wa kupiga kura kuchagua saa ambayo mkutano wa kwanza wa wanablogu wa Tanzania utafanyika kama alivyoeleza Jeff Msangi. Kwahiyo inabidi wasimamizi wa uchaguzi wasilale kabisa kuhakikisha kuwa masanduku ya kura hayaibiwi! Zaidi kuhusu mkutano huu msome Jeff:hapa na hapa, na Egidio: hapa na hapa. Bonyeza hapa upige kura yako. Bonyeza hapa ushiriki kupanga ajenda za mkutano. Ni muhimu sana kwa wale wote wanaotaka kushiriki kutoa mawazo yao juu ya mambo ya msingi ya kujadili na pia muda wa mkutano wenyewe. (bonyeza hapo chini umalize kusoma ukurasa huu).
(more…)
Thu 9 Nov 2006
Katika majadiliano na Jeff, imeonekana kuwa sio vyema tukasubiri hadi siku ya mkutano bila kuwa na ajenda. (Kama hujui nazungumzia mkutano gani bonyeza hapa na hapa). Tunaweza kupoteza muda mwingi kwa kuzungumzia mambo ya kila aina. Tukaenda huku na kule na kurudi huku. Bila kichwa wala…niseme mkia? (binadamu tuna mikia?). Haya, bila kichwa wala miguu. Basi ili kutunza muda siku hiyo tafadhali shiriki kujadili ajenda za kujadiliwa, mkutano ufanyike kwa muda gani (saa moja? moja u nusu, masaa mawili?, n.k.). Kama alivyosema Jeff, hakuna sababu za watu fulani kuandaa ajenda kwa ajili ya watu wengine. Tunatakiwa kuanza kujenda utamaduni wa demokrasia ya ushirikishwaji. Hivyo tunapaswa wote kushiriki kuamua ajenda za kujadiliwa. Ili ushikiri, bonyeza hapa, uende kwenye ukurasa wa wiki ambao utaweza kushirikiana na wengine kupanga ajenda za siku hiyo. Maelezo ya jinsi ya kutumia ukurasa wa wiki sio magumu: ukitaka kubadili, kuhariri, au kuongeza jambo, bonyeza panaposema “edit” juu ya kipengele ambacho unataka kukifanyia kazi. Kwahiyo ukitaka kuweka jambo kwenye kipengele cha ajenda, bonyeza “edit” juu ya neno “ajenda.” Kisha andika, halafu bonyeza pale chini panaposema, “save page.”
**Muhimu: ukitaka kuweka jambo kwenye ukurasa wa wiki, bonyeza panaposema “edit” JUU ya hicho kipengele. Usibonyeze “edit” popote pale. Kila kipengele kina neno hili “edit” upande wa juu kulia. Ukipata tatizo usisite kuuliza.
Thu 9 Nov 2006
Nia kubwa ya makampuni ya kibiashara ni kuzalisha faida. Lakini, je makampuni haya yana wajibu wowote kwa jamii? Dhana inayoelekea kupata nguvu sana siku hizi iitwayo “corporate social responsibility” inaelezea wajibu wa kijamii ambao makampuni yanapaswa kuwa nao. Baada ya mjadala kuhusu Umoja wa Mataifa (mwanamuziki Fela Kuti alikuwa akiuita umoja huu: Dis-United United Nations!) mwezi wa tisa mwaka huu, shirika la habari la Uingereza, Reuters, litaendesha mjadala mwingine leo kuhusu hii dhana ya uwajibikaji wa kijamii kwa makampuni ya kibiashara. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii)
(more…)
Sat 4 Nov 2006
Hivi ukiandika hadithi kwa kiingereza na Kiswahili kwa wakati mmoja itakuwaje? Msome mwanablogu wa Tanzania Sandra Mushi upate jibu. Bonyeza hapa.
—-
Jeff ameandika zaidi kuhusu ule mkutano wa wanablogu na wapenzi wa blogu wa Tanzania. Bonyeza hapa usome nyongeza yake, bonyeza hapa usome akiwasilisha hoja na kuelezea juu ya umuhimu wa kukutana, na bonyeza hapa usome niliyoandika kuhusu jinsi ya kupanga siku na saa za kukutana na mahali tutakapokutania.
Thu 2 Nov 2006
Na Ndesanjo Macha, Maudhui:
skolashipu ,
mikutanoToa Maoni [1]
Samahani, taarifa hii inakuja kukiwa kumebaki siku moja! Lakini taratibu za kuomba hazina mambo mengi hivyo unaweza kutumia saa moja hivi kuweza kutuma maombi yako. Skolashipu hii ni ya kujumuika na watu wengine wanaotazama kwa undani masuala ya teknolojia, vyombo vya habari na vile vya uongo, na jamii. Huu ni mkutano wa tatu wa kila mwaka wa We Media. Mkutano wa kwanza ulifanyika kule Yoku Mpya (New York) ambapo nilipata nafasi ya kuhudhuria. Bonyeza hapa, hapa, hapa na hapa usome niliyoandika kuhusu mkutano huo wa New Cork. Mwaka huu mkutano ulihamia Uingereza. Bonyeza hapa usome niliyoandika kuhusu mkutano wa mwaka huu. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
(more…)
Thu 2 Nov 2006
Sina neno la kuongeza kuelezea kwanini wanablogu wa Tanzania tunahitaji kukutana. Jeff Msangi ameelezea vizuri na baadhi ya wanablogu tayari wametoa maoni kuunga mkono hoja yake. Namshukuru kwa jitihada zake za kutaka tukutane, mtandaoni kwa hivi sasa, wakati tukisubiri siku ambayo tutakaa meza moja, kula, na kucheka pamoja. Kama hujamsoma Jeff akitoa wazo la mkutano huu, bonyeza hapa.
Sasa ili kufanikisha mkutano wenyewe, kuna mambo mawili tunatakiwa kufanya. Jambo la kwanza ni kukubaliana kuhusu siku na saa. Kutokana na ukweli kuwa tumetapakaa katika nchi mbalimbali na hivyo masaa yanatofautiana, inatupasa kuchagua saa kwa makini sana. Kibinafsi ningependa sana tutilie mkazo hali halisi ya wenzetu walioko nyumbani. Kwa mfano, ni rahisi kwa walio Ughaibuni kushikiri kwenye mkutano huu usiku wa manane au matisa kuliko wenzetu walioko Tanzania. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii).
(more…)