NEWS: Discount viagra europe Discount phentermine prescription Discount viagra perscription drug Order phentermine on line? 92 accepted cod phentermine Compare viagra prices, Pharmacy online phentermine Purchase tramadol online. Phentermine sites that ship cash on delivery Viagra retail discount Home made viagra Valium vs xanax Xanax no prescription Viagra sales online Erection viagra Free viagra without prescription Phentermine fda Xanax withdrawl Effects phentermine side strong Information viagra woman What does phentermine do to your heart Long term phentermine use Viagra testimony Phentermine very cheap Buying phentermine Cialis pill? Discount online phentermine Buy cheap phentermine yellow Tramadol hcl tab Phentermine hydrochloride ship to missouri: Buy viagra prescription online Compare phentermine prices Cialis compare levitra viagra Picture of generic xanax Tramadol uses Recreational viagra use Generic india viagra Cheap viagra generic Cialis drug Natural phentermine Phentermine cheapest price 5 no perscription! Cialis and pomegranate interaction Viagra for woman? Ionamin phentermine Cheapest xanax online! Xanax drug interactions Buy cod phentermine Phentermine online Methadone and xanax Recreational viagra Viagra online sales Mexican phentermine Cod tramadol! Phentermine mexican pharmacies online Phentermine pictures Cheap phentermine without a prescription Compare viagra cialis levitra. Xanax master card Long term effects of xanax, Viagra cialis levitra comparison dosages Does viagra woman work 5 in round white tablets no imprint code 50 mg viagra Phentermine shipped cod Phentermine for less Viagra information Phentermine free consultation? Viagra kaufen Is tramadol a narcotic Cheap quality viagra Phentermine and topiramate for weightloss Diet loss phentermine pill weight Diet phentermine pill sale Kevin harvick viagra Xanax withdrawls Purchase viagra online Cialis new viagra. Viagra for woman information Online ordering viagra Viagra prescription uk Buying phentermine: Can i take xanax with zocor and procardia Phentermine overnight Does viagra work Low natural resources for the drug phentermine Viagra treatment migraine headache Buy in online uk viagra, Apcalis cialis 180 phentermine Black market costa rica pharmacy phentermine no imprint code Buying tramadol online Loss phentermine story success weight How much weight will you lose on phentermine Online xanax prescription Cialis compared to viagra Paxil with phentermine interactions Xanax addiction treatment. 0 buy by popl powered viagra wordpress Cheap tramadol 180 Viagra in woman Lethal doses of klonopin and xanax Stopping xanax Cialis overnight! Phentermine and urine drug screen Smoking xanax: Ingredient phentermine Saturday delivery phentermine Viagra prescription medication Free cialis 25 mg Viagra uses Xanax detoxification Viagra pictures Pfizer viagra online Online adipex phentermine prescriptions. Side effects of tramadol hydrochloride On line prescription viagra 100 phentermine Female spray viagra Tramadol hc Free viagra sample I need to find cheap phentermine delivered to fl Online pharmacy phentermine xenical meridia Compare phentermine prices Canada cialis generic? Xanax shipped cod No perscription xanax cheap Acquisto cialis Generic india viagra Buy cheap purchase uk viagra Viagra price Online phentermine pharmacy best cheapest Tramadol 50mg. Buy viagra online get prescription Addiction recovery xanax, Price for generic viagra Diet inexpensive phentermine pill Generic viagra canada No prescription phentermine Phentermine withdrawal symptoms Cheap viagra order online Cheapest viagra price Phentermine online doctor prescribed? Buy cialis uk Fast delivery phentermine, Keyword prescription qoclick tramadol without Tramadol dog Phentermine wholesale Snorting phentermine Discount phentermine online Tramadol online Cheap tramadol no prescription Cialis comparison levivia viagra Cheapest viagra online 92 accepted cod phentermine Cheap phentermine with online consultation Viagra alternatives uk Buy prescription tramadol without Buying viagra in the uk Xanax description Oxycontin xanax bars perclesept and lortab wha Generic viagra cialis Generic lowest price viagra Phentermine at cost with no prescription Picture of xanax pill Phentermine shortage Phentermine cheap free shipping Phentermine yellow 30 mg Addiction tramadol Tramadol hydrochloride tablet Phentermine cod delivery Online phentermine order Cyber pharmacy viagra Dangers of phentermine heart Buy cheap tramadol Xanax alcohol Cialis generic Tramadol prescription Free phentermine prescriptions 50 mg viagra Phentermine studies Viagra and levivia Phentermine feedback How long between phentermine and meridia Low cost phentermine Phentermine and topiramate for weightloss Tramadol hc Viagra overnight delivery Phentermine success stories Viagra cheap prescription Tramadol hydrochloride capsules Free shipping phentermine Diet pill addiction phentermine? Generic cialis soft tabs Side effects of xanax xr: Phentermine quick Buy xanax on line How long does xanax stay in the system Importing cialis from canada to us Buy cheap domain onlineatspacecom xanax Phentermine and diet pill

December 2006


Habari fupi niliyoandika kuhusu “Person of the Year” nimeitia minofu zaidi na hivyo kuwa makala ndefu ambayo imechapwa kwenye gazeti la Mwananchi la tarehe 31, Desemba 2006. Bonyeza hapa uisome. Katika toleo hilo kuna makala kiboko aliyoandika Freddy Macha kuhusu mwanamuziki wa Tanzania, Vitali Vitalis Maembe, na mwanamuziki aliyefariki hivi karibuni, James Brown. Tafadhali soma makala hii. Nimeirudia mara mbili. Isome mwenyewe, utaniambia. Bonyeza hapa. Unaweza pia kusikiliza wimbo wa Vitali Vitalis uitwao Sumu ya Teja katika ukurasa wake wa Myspace. Sikiliza nyuzi anavyozidonoa. Na ngoma zile zikimsindikiza. Pia bonyeza hapa utazame video ya wimbo wake wa Salaam Aleykhum (shukrani Gotta kwa kiungo hiki). Dakika chache zilizopita nilikuwa nasikiliza wimbo wa Kilimanjaro wa Freddy Macha. Midundo yake ilinifanya niwe nacheza huku nikiandaa chai. Bonyeza hapa uusikilize.

**Msomaji Gotta katupatia kiungo chenye maneno ya wimbo wa Vitalis wa Sumu ya Teja. Bonyeza hapa uyasome.

Kama wewe ni mpiga picha au mwanablogu wa picha, bonyeza hapa usome jinsi utakavyoweza kuuza picha zako. Kwa wale wanaopenda kujenga tovuti zao wenyewe ila hawana ujuzi au muda wa kujifunza toka A hadi Z, bonyeza hapa. Kisha kama wewe ni mwanablogu na unapenda kutumia huduma inayopiga picha tovuti au blogu ambazo umeweka viungo vyake katika mambo unayoandika (kama unavyoona inavyokuwa katika viungo nilivyoweka hapa), bonyeza hapa. Hizi zote ni makala fupi mpya nilizoweka kwenye Mwongozo wa Wanablogu.

Nilipokwenda India, ukiacha suala la kusafisha macho, nilihudhuria mikutano miwili. Mikutano hii ni ule wa Global Voices Online na wa pili uliitwa Hibiscus Project. Mkutano wa Global Voices ulifanyika kwa siku mbili. Nilijaribu, ingawa mtandao-usiwaya uliniangusha, kuandika yaliyojadiliwa siku ya kwanza ya mkutano huo. Bonyeza hapa usome niliyoandika toka ndani ya mkutano (jua kuwa niliandika bila kupitia na kuna mambo mengi pia ambayo yalinipita sikuyaandika). Siku ya kwanza ilikuwa wazi kwa mtu yeyote ambaye alikuwa amejiandikisha. Mkutano wa siku ya pili ulikuwa ni wa wahusika wakuu wa mradi huu ambapo masuala ya ndani yalijadiliwa. (more…)

Nilipokuwa India nilisema kuwa huenda dunia haijapata kuwa na madereva makini (na wanaoendesha kwa fujo wakati huo huo) kama madereva wa India. Huenda ulidhani kuwa ninatania au ninakuongopea. Sasa kuna ushahidi ujionee mwenyewe. Madereva wale sitakaa niwasahau. (more…)

Kuanzia tarehe 26 Desemba hadi tarehe 1 Januari baadhi ya watu wenye asili ya Afrika Marekani na kwingineko duniani husherehekea sikukuu ya Kwanzaa. Ni kipindi cha kutafakari masuala ya familia, historia, utamaduni, na jumuiya kwa kupitia dhana ya Nguzo Saba. Ni kipindi cha kusalimiana kwa Kiswahili, “habari gani,” “nzuri.” Sitaandika kipya, nitakachofanya ni kuchimba ndani ya blogu yangu na kuibua mambo niliyoandika huko nyuma juu ya siku hii. Hii tabia ya kuanza kuchimba mambo ya nyuma naanza kuipenda (ingawa inaweza kufanya mtu ukawa mvivu wa kuandika mapya. Lakini ina utamu wake, jaribu utaona). Makala ya kwanza kuhusu Kwanzaa inaitwa “Kwanzaa: Meza ya Umoja (na khanga za Mnazi Mmoja).” Bonyeza hapa uisome.

Makala ya pili kuhusu Kwanzaa inaitwa “Somo, Ngoma, na Tambiko la Kwanzaa.” Bonyeza hapa uisome. Tafadhali tafakari kuhusu Nguzo Saba za Kwanzaa.

Kila mwaka gazeti la Marekani la Time huwa linachagua mtu ambaye huitwa “Person of the Year.” Wakati mwingine huweza kuwa ni mtu zaidi ya mmoja. Kwa mfano, mwaka jana walichaguliwa mwanamuziki Bono, Melinda Gates na mumewe Bill Gates. Huko nyuma walikuwa wakitumia maneno “Man of the Year” wakati ambapo kuna wakati watu waliochaguliwa walikuwa ni wanawake. Basi baadaye wakabadili kuwa “Person of the Year.” (more…)

Uchovu usio na kifani. India, nitarudi tena. Nitakukumbuka daima. Nipumzike kwanza kabla ya kukupa picha halisi ya safari ya India na pia taarifa zaidi za mkutano wa Global Voices (ambao ndugu Egidio alishiriki na kupewa nafasi ya kuongea kwa Kiswahili mbele ya washiriki wote kwa dakika chache). Wakati napumzika, ningependa kukuacha na tafakari ya huu “mkumbo wa kadamnasi” uitwao Krisimasi. (bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii):

(more…)

Ndio jibu ninalowapa watu ninapokuwa nakatiza mitaa fulani fulani hapa India ambayo imekaakaa kinamna. Hii ni mitaa ambayo wenyeji wananiambia niwe macho nikipita huko. Basi nikipita mitaa hiyo nikiulizwa nafanya kazi gani mimi huwaambia kuwa ninafundisha Kung-Fu. Mimi eti ni mwalimu wa Kung-Fu. Kisha nawaonyesha mbwembwe kidogo kama za Bruce Lee akiwa kwenye sinema ya Enter the Dragon na kuwauliza kama wanamfahamu. Wengi wanasema wanamjua, basi nawaambia kuwa mimi hufundisha watu kupigana kama Bruce Lee! (more…)

Ukipewa maji ya kunywa yaliyoko ndani ya chupa ukiwa jijini Delhi, haina maana kuwa hayo maji ni yale “spesho.” Inawezekana kabisa kuwa ni maji yaliyochemshwa kisha yakawekwa ndani ya chupa za maji ya dukani! (more…)

Bonyeza hapa utazame picha za tarakilishi ya mapajani ya watoto kwa ajili ya nchi zinazoendelea iliyoletwa kwenye mkutano wa Global Voices, jijini New Delhi. Picha hizi kapiga mwanablogu Egidio. (more…)

Bado ulimi wangu unawaka moto. Pilipili. Acha tu. Basi ukija India mitaa niliyokatiiza ukaniulizia kwa jina la ndesanjo, hutanipata. Baada ya kuona kuwa kwa Wahindi wengi hata neno Tanzania ni gumu kutamka, basi niliamua kuwaambia kuwa naitwa Gandhi! Ukija ulizia kama wanamfahamu yule Gandhi wa Afrika. Watakwambia, “Aah, tunamjua. Alikuwa akipita hapa kijiweni usiku na kutuuliza maswali kibao na kutaka kujifunza kihindi.” Basi ndio mimi huyo. Wanaweza pia kukwambia kuwa mifuko ya suruali yangu ilikuwa imetunatuna. Ila hawajui kuwa mfukoni nilikuwa nimeweka bisibisi, mawe, na zana nyingine za kujilinda!!Nikijitokeza barabarani dakika hiii, utasikia madereva teksi na wachuuzi wakiita, Gandhi, Gandhi, Gandhi! Wananifurhia kiasi ambacho nadhani hadi ukifika wakati wa kuondoka nitakuwa nimeshapewa mungu wangu! Unakumbuka nilikwambia kuwa India ina miungu wanaozidi idadi ya watu hivyo hawataluwa na uchoyo wa kunipa mungu mmoja au wawili. Nami sitakataa. (more…)

Habari hii, Hii Ndio India, ningependa kuiwekea viungo kadhaa lakini sina subira hata kidogo. Mtandao hauna kasi kabisa. Viungo nitaweka wakati mwingine. Msome Mental Acrobatics na pia Egidio ambao walikuwa kwenye mkutano leo hii hapa Delhi. 

—— 

Hii ndio India. Naambiwa.
 
Toka niwasili tayari nimekaribia kugongwa na magari mara kadhaa, nimeshikwa shati na ombaomba, na karibu niingizwe “mjini.”
 
India nchi ya aina yake.
 
Sanamu za miungu wa Kihindi na mahekalu yamejaa kila kona. Kuna mitaa ya India ina mahekalu madogo (mengine yana ukubwa wa kujaa watu wawili!). Ukifika uwanja wa ndege wa Delhi, kitu cha kwanza unachokutana nacho ni sahamu ya mungu wa Kihindi, Kali. Mungu huyu ni hatari sana, kazi yake ni kuangamiza watu wabaya. Sio tu India ina idadi kubwa ya sanamu za miungu kuliko nchi yoyote duniani, bali pia ina miungu wengi kushinda hata idadi ya wahindi wenyewe! India ina watu wapatao bilioni moja. Idadi hii ni ndogo ukilinganisha na miungu wao. Kila kijiji kina miungu wake! (bonyeza hapo chini umalie kusoma)
 

(more…)

Haya ni mambo niliyoandika wakati mkutano wa Global Voices ukiendelea. Nilikuwa niweke hapa kadri mkutano ulivyokuwa ukiendelea ila kutokana na tatizo la mtandao nikashindwa. Kwakuwa nilikuwa nimepanga kupandisha mambo haya bila kusahihisha chochote, na kwakuwa sina muda wa kufanya hivyo, ninapandisha mambo haya hivyo hivyo. Tembelea pia blogu ya Egidio ili upate habari za mkutano huu, bonyeza hapa. Egidio: ilikuwa furaha kubwa kukutana nawe! (bonyeza hapo chini umalize kusoma).

(more…)

Nyongeza: nimekuwa najaribu kuingia kwenye Intaneti kwa zaidi ya saa moja bila mafanikio. Nilisahau kuweka kiungo ambacho kitakusaidia kuweza kushiriki na hata kutuma maswali kwenye mkutano huu. Bonyeza hapa.

Pia unaweza kufuatilia video ya moja kwa moja toka mkutanoni kwa kubonyeza hapa na kufuata maelezo utakayoyakuta hapa.

——-

Mkutano umeanza. Tatizo la mtandao usiwaya wa Intaneti ambalo limekuwa likitusumbua sana toka tufike hapa India bado linaendelea. Tatizo hili ndio limenifanya nikashindwa kuandika toka nifike hapa. Kila ninapofanikiwa kupata mawasiliano ya Intaneti ninachoweza kufanya ni yale mambo machache.

Hapa mkutanoni napo tatizo linaendelea. Lakini ukiacha tatizo hili nina furaha kubwa kuwa mwanablogu wa Kiswahili Egidio Ndabagoye yuko hapa mkutanoni. Amekaa kona ya kulia, viti kadhaa toka nilipokaa mimi. Na ataongea kwa Kiswahili na wana mkutano hapo baadaye. Wanablogu toka nchi mbalimbali wataongea kwa lugha tofauti katika kuonyesha kuwa “global voices” ziko katika lugha mbalimbali. Basi Egidio ataongea kwa Kiswahili.

Pia hapa ndani kuna mwanablogu toka Kenya, Mental Acrobatics na mwanablogu toka Uganda, Ishna.

*Kwakuwa naandika haraka huku nikishiriki kwenye mkutano, naweza kukosea herufi na pia naweza nisiwe na nafasi ya kuweka viungo na mambo kama hayo. Nitasahihisha baadaye.

Sahihisho: wanablogu wa Kiswahili watakaohudhuria mkutano huu huenda bado wakawa wawili, ingawa Nambiza hatakuwepo. Mwanablogu Egidio wa Pilikapilika Vyuo Vikuu kuna uwezekano mkubwa naye akawepo.

——

Ninasikitika sana kuwa ndugu Nambiza Tungaraza hataweza kuhudhuria mkutano wa Global Voices Online kule New Delhi, India kutokana na sababu fulani fulani za kibinafsi. Tulikuwa tuwe na wawakilishi wawili wa blogu za Kiswahili kwenye mkutano huu. Ingekuwa poa sana kukutana nawe Tunga. Mara ya mwisho mwaka gani vile?…miaka ya tisini nadhani. Ilikuwa pale nyumbani kwenu, kisha ufukweni na ndugu Kibope na lile gitaa kavu. Kuna wimbo ule mlikuwa mmeutunga, nimeusahau jina. Miaka imepita. (bonyeza hapo chini umalize kusoma).

(more…)

Nyongeza: sura za wana Global Voices watakaokuwa New Delhi, bonyeza hapa.

———

Jumanne wiki hii ninasafiri kwenda New Delhi, nchini India kushiriki kwenye mkutano wa kila mwaka wa mradi wa Global Voices Online:

Global Voices Online is an award-winning online portal and guide to international blogs beyond North America and Western Europe. It has also become the hub of a growing community of international bloggers who want to build a better global conversation.

(bonyeza hapo chini umalize kusoma habari hii)

(more…)

Zawadi ya miaka 45 ya “uhuru” wa Tanganyika toka kwa mwanablogu wa katuni, Musa NgarangoBonyeza hapa upokee zawadi hii.

Waziri Mkuu ndugu Lowassa hebu acha utani.

Nimepitia la The Guardian nikakuta habari ina kichwa hiki: Lowassa Calls a Spade a Spade. Nikadhani ni habari moto na nzito hasa. Namaliza kuisoma nikitikisa kichwa. Maswali anayouliza Waziri Mkuu huyu ni maswali ambayo sisi wapiga kura tungepaswa kumuuliza. Pengine kwakuwa hatumuulizi basi akaamua kujiuliza mwenyewe. (bonyeza hapo chini umalize kusoma).

(more…)

Nilikuwa napitia mambo niliyokuwa naandika wakati nilipoanza kublogu. Nadhani ni jambo zuri ukishablogu kwa muda kupitia mambo ya nyuma. Sasa nimekuta habari mbili nilizoandika mwaka 2004, zote ni fupi fupi. Ya kwanza nilikuwa nikiongelea suala la hofu tuliyonayo ya kuhoji mambo: Hoji, Usiogope. Bonyeza hapa uisome. Nyingine ni visa vya jiji la Dasalama kwa Kaka Dito! Bonyeza hapa usome, Oya, Shika Mchuma!

Sultan Tamba kumbe mtu wa matani namna hii. Sikujua. Ukiacha kamera, ndugu Tamba ni mchoraji mahiri kama utakavyoona katika katuni aliyochora kuonyesha masahibu yaliyowakumba wajumbe walioshindwa kuingia ndani ya ukumbi wa mkutano wetu. Bonyeza hapa uitazame. Kwakuwa nimemtaja Sultan Tamba ambaye ni mtengeneza filamu, ngoja nikuulize kama unafahamu kuhusu Bongowood. Kama jinsi ambavyo kuna Hollywood, na baadaye ikaja Bollywood, ikafuatia Nollywood, sasa kuna Bongowood. Bonyeza hapa.

Next Page »