Baada ya kurudi Afrika na kuzama kwenye shughuli zilizonitoa kidogo nje ya blogu na masuala mengine mtandaoni, nimeibukia Tshwane (jina jipya la Pretoria) nikajisikia kama vile nilikuwa nje ya dunia hii. Pale Tshwane nilishiriki kwenye warsha iliyoitwa Pan African Localisation Workshop. Hii ni warsha iliyokuwa ikiwashirikisha watu mbalimbali toka Ethiopia, Djibouti, Msumbiji, Nigeria, Ghana, Misri, Marekani, Tanzania, Uswisi, Congo (DRC) na Senegal ambao wanajihusisha na masuala ya lugha na teknolojia, hasa masuala ya kuenyejisha (localise) zana/programu za kompyuta na maarifa mtandaoni. Mradi huu umefikisha mwaka wa tatu toka uanze kufadhiliwa na IDRC.

The PanAfrican Localisation project is a three-year effort, funded by IDRC, to build capacity for localisation in African languages including Arabic.

(more…)