Makala kuhusu teknolojia ya blogu nilizozungumzia jana (bonyeza hapa kama hukusoma niliyoandika jana) ninaziweka hapa ili zisomwe na wale ambao walipitwa na gazeti la Mwananchi au ambao wako Ughaibuni. Makala hizi, ziko katika sehemu tatu, niliandika kwa ajili ya safu yangu ya kila jumapili katika gazeti hilo. Kwa wanablogu, mambo mengi niliyoandika mnayafahamu. Tumekuwa tukiyazungumza mara kwa mara. Sikuandika kwa ajili ya watu ambao tayari ni wanablogu maana ingekuwa ni sawa na “kuhubiria wanakwaya.” Niliandika kwa ajili ya watu ambao hawajui teknolojia hii au ambao wanaisikiasikia. Haya, hizi hapa (bonyeza juu ya vichwa vya habari uzisome): Ndesanjo, Hivi Blogu ni Nini? – 1, Ndesanjo, Hivi Blogu Ni Nini? – 2, Ndesanjo, Hivi Blogu Ni Nini? - 3