Wakati naelekea kwenye mkutano wa jumuiya ya wana Wikipedia, Wikimania (bonyeza hapa usome nilipouzungumzia mkutano huo huko nyuma [hivi kuna aliyeomba zile skolashipu?]), tunaambiwa kuwa mwanablogu wa video mwenye umri wa miaka 24 katiwa lupango kwa kukataa kutoa mikanda ya video. Soma habari hiyo katika viungo vifuatavyo: hapa, hapa, na hapa.

Kati ya watu watakaotoa mada katika mkutano huo ni ndugu Martin Benjamin, mwanzilishi wa kamusi huria ya mtandaoni, Internet Living Swahili Dictionary. Mada yake inasema: Huru na Bure: Swahili Collaboration and the Future of African Languages on the Web. Kama unakereketwa na masuala ya programu huria, kamusi huria, kamusi elezo huria, n.k.. Fuatilia habari za Wikimania hapa.