Unajua kuna watu ambao wanadhani kuwa sisi Waafrika hatuwezi. Utawasikia wakisema, “wazungu achaneni nao.” Kumbe suala sio rangi. Ni mazingira, sera, na kuwezeshwa kwa wanafunzi, wanazuoni, na wananchi kwa ujumla. Blogu ya Afrigadget inasaidia kuondoa hisia potofu kuwa sisi Waafrika hatuwezi. Sio wanasayansi. Sio wabunifu. Sio wavumbuzi. Uwe ukiitembelea blogu hii kupata habari mbalimbali kuhusu wanasayansi wetu ambao hakuna anayewajali. Hata zile wizara zinazoitwa “wizara za sayansi” (na utumbo) hazina hata majina yao. Afrigadget inatupa habari na picha ya baiskeli yenye injini kama pikipiki iliyotengenezwa Mombasa, Kenya.