Muhtasari wa blogu za Kiswahili katika GV toka kwa Mwandani. Bonyeza hapa.
——-
Muda mfupi uliopita nimepata taarifa toka kwa White African ya zana iliyoundwa na jirani zetui wa Kenya iitwayo Jahazi. Bonyeza hapa ujionee mwenyewe. Unajua zama za mapinduzi ya viwanda ulikuwa huwezi kushindana na “mzungu” maana mtaji uliohitajika wakati ule ulikuwa ni mkubwa, zama hivi za habari na mawasiliano, tunashikana mashati. Unachohitaji sana sana ni fikra na ubunifu. Jahazi imeundwa Kenya na inahifadhiwa Kenya.